KATIBU MKUU MAKONDO, UNICEF WAJADILI NAMNA YA KUIMARISHA ULINZI WA HAKI ZA MTOTO


 


 XXXXXXXXXXXXXX

Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Bi. Mary Makondo amekutana na ujumbe wa wawakilishi kutoka UNICEF ukiongozwa na Mkuu wa Ulinzi wa Mtoto, Bi. Maud Droogleever Fortuijn na kujadili namna watakavyoshirikiana  kuimarisha ulinzi wa haki kwa mtoto.

 Bi. Makondo amewahakikishia UNICEF kuwa Wizara ya Katiba na Sheria itaendelea kushirikiana na wadau kuhakikisha kuwa haki za watoto zinalindwa, 

Aidha ameahidi kuwa wadau watashirikishwa katika hatua zote za maboresho ya mfumo wa haki jinai.

 Mkutano huo ulifanyika katika ofisi za RITA Jijini Dar es Salaam, tarehe 8 Julai, 2022.

 


Comments

Popular posts from this blog

USAJILI WA VIZAZI NA VIFO NI TAKWA LA KISHERIA

UONGOZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA YA HAKI ZA BINADAMU NA WATU YAKUTANA NA VIONGOZI WA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA

BODI YA KITAIFA YA USHAURI YA MSAADA WA KISHERIA YATEMBELEA WASAIDIZI WA KISHERIA IRINGA