MAPAMBANO DHIDI YA DAWA ZA KULEVYA YAWE ENDELEVU - WAZIRI NDUMBARO


 


XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX



Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) , Waziri wa Katiba na Sheria amesema mapambano dhidi ya dawa za kulevya yanatakiwa kuwa endelevu.

Dkt. Ndumbaro amesema hayo kwa niaba ya Mhe. George Simbachachene, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera,Bunge na Uratibu) wakati akimkaribisha Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb), Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kufunga rasmi maadhimsho ya kitaifa ya Siku ya Kupambana na Dawa za Kulevya Duniani yaliyofanyika tarehe 1-2 Julai, 2022 Viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam.

"Dawa za kulevya zina madhara makubwa kwa ustawi wa jamii, Maendeleo ya Nchi na Dunia kwa ujumla, hivyo mapambano dhidi ya matumizi ya dawa za kulevya yanatakiwa kuwa endelevu" alisema Dkt. Ndumbaro.

Comments

Popular posts from this blog

USAJILI WA VIZAZI NA VIFO NI TAKWA LA KISHERIA

UONGOZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA YA HAKI ZA BINADAMU NA WATU YAKUTANA NA VIONGOZI WA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA

BODI YA KITAIFA YA USHAURI YA MSAADA WA KISHERIA YATEMBELEA WASAIDIZI WA KISHERIA IRINGA