SERIKALI YAZUNGUMZA NA WATAALAM WA HAKI ZA BINADAMU (SPECIAL RAPPORTEURS) WA UMOJA WA MATAIFA


 


 XXXXXXXXXXXXXXXX

Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Damas Ndumbaro ameongoza kikao na Wataalam wa Haki za Binadamu (Special Rapporteurs) wa Umoja wa Mataifa wanaoshughulikia masuala ya watu asilia (indigenous people) na makazi.

 

Dkt. Ndumbaro alitumia fursa hiyo kawaalika nchini Tanzania wataalam hao wa haki za binadamu

 

"kwa niaba ya Serikali nawakaribisha sana mje kutembelea Tanzania na mpate fursa ya kujionea vivutio vya utalii, tamaduni zetu na utofauti wa mila mbalimbali za makabila zaidi ya 100 yaliyopo Tanzania" alisema Dkt. Ndumbaro

 

Wataalam hao wamepongeza jitihada za Serikali katika kutekeleza haki za binadamu hususani fidia waliyowapatia waliokuwa wakazi wa Ngorongoro na kuhamia Msomera wilayani Handeni kwa hiyari yao. Aidha, wameahidi ushirikiano zaidi na Serikali ya Tanzania katika masuala mbalimbali yanayohusu haki za binadamu.

 

Mkutano huo uliofanyika kwa njia ya mtandao tarehe 8 Julai, 2022 jijini Arusha, ulihudhuriwa pia na Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Prof. Eliamani Sedoyeka pamoja na watendaji kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii na watendaji kutoka Wizara ya Katiba na Sheria.

 


Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YAIPONGEZA WIZARA KWA UTEKELEZAJI WA MAMA SAMIA LEGAL AID CAMPAIGN

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA