WANANCHI MSISUBIRI MATUKIO YA KITAIFA PEKEE KUTAFUTA HUDUMA KWANI VYETI VYA KUZALIWA VINATOLEWA SIKU ZOTE- WAZIRI NDUMBARO


 

XXXXXXXXXXXXXXXXX 

Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt Damas Ndumbaro leo tarehe 6 Julai ,2022 ametembelea na kukagua zoezi la usajili na kuwapatia vyeti vya kuzaliwa Wananchi linaloendelea katika viwanja vya Maonesho ya biashara ya Kimataifa Sabasaba Jijini Dar es salaam.

 

Akiongea na Wananchi waliokuwa wakipatiwa huduma hiyo Mhe, Dkt Ndumbaro amewataka kuwa mabalozi watakaporudi majumbani mwao Kwa kuwaeleza ndugu, jamaa na majirani zao kuhusu umuhimu wa kusajili amatukio ya vizazi na vifo, ndoa na talaka na mengineyo kwa wakati badala ya kusubiri maonesho au matukio yanayowakusanya kwa mwaka mara moja.

 

‘’Sasa hivi huduma zimesogezwa karibu yenu kwa upande wa watoto wa umri chini ya miaka mitano wanasajiliwa katika ofisi za kata na vituo vya tiba vinavyotoa huduma ya mama na mtoto katika Mikoa 23 na kwa upande wenu watu wazima unaweza kujisajili kielektroniki sehemu yoyote ulipo Kisha ukapata cheti chako Kwa wakati muafaka’’ Alisema Mhe. Dkt Ndumbaro.

 

Kwa upande wake Kabidhi Wasii Mkuu na Afisa Mtendaji Mkuu Bi. Angela Anatory amesema mwitikio ni mkubwa wa wananchi wanaofika kupatiwa huduma ya usajili ili wapatiwe vyeti vya kuzaliwa hivyo kuwatoa Wasiwasi Kwa kuwa watoa huduma wamejipanga kuhakikisha kila mwenye sifa ya kusajiliwa anapatiwa huduma hiyo.

 

‘’Wananchi wamejitokeza na nimezungumza na baadhi yao wamepongeza na yapo maeneo yenye changamoto tumeyachukiwa na tutayafanyia kazi Kwa haraka, nashukuru tangu tulipoanza tarehe 29 Juni, 2022 hadi leo tarehe 6 Julai,2022 tumesajili Wananchi 3,000 na idadi hiyo itaongezeka kwani wananchi wanaendelea kupatiwa huduma huyo’’. Alisema Bi. Anatory.


Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YAIPONGEZA WIZARA KWA UTEKELEZAJI WA MAMA SAMIA LEGAL AID CAMPAIGN

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA