WAZIRI NDUMBARO ATAKA KASI YA UJENZI JENGO LA WIZARA IONGEZWE


Waziri wa Katiba na Sheria Dk. Damas Ndumbaro, akizungumza mara baada ya kukagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Wizara hiyo katika Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma Juni 30, 2022.

Waziri wa Katiba na Sheria Dk. Damas Ndumbaro, akitoa maelekezo kwa wasimamizi wa mradi wa ujenzi wa  Jengo la Ofisi ya Wizara hiyo mara baada ya kufanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi huo  katika Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma Juni 30, 2022.




Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe.Geophrey Pinda, akizungumza mara baada ya Waziri wa Katiba na Sheria Dk. Damas Ndumbaro (hayupo pichani) kukagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Wizara hiyo katika Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma Juni 30, 2022.
Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Bi. Mary Makondo, akimshukuru Waziri wa Katiba na Sheria Dk. Damas Ndumbaro kwa kufanya ziara ya kukagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Wizara hiyo katika Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma Juni 30, 2022.

XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX


Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro aagiza kasi ya ujenzi wa Jengo la Wizara ya Katiba na Sheria linaloendelea kujengwa katika mji wa Serikali Mtumba Jijini Dodoma iongezwe ili jengo likamilike kwa wakati.

 

Agizo hilo amelitoa leo tarehe 30/06/2022 wakati Waziri Ndumbaro alipofanya ukaguzi wa ujenzi wa jengo hilo.

 

Waziri Ndumbaro amesema “Tumekagua na tumeona kazi inavyoendelea lakini hairidhishi, nasisitiza Mkandarasi ongeza kasi ya ujenzi na Mshauri Mwelekezi ongeza usimamizi”

 

Aidha, Waziri Ndumbaro alimuagiza Meneja wa mradi, Mkandarasi na Mshauri Mwelekezi kufikia tarehe 06, Julai, 2022 wawasilishe kwa Katibu Mkuu wa Wizara taarifa inayoelezea ni lini jengo hilo litakabidhiwa kwa Wizara na kama kuna maombi ya kuongezewa muda waeleze wanataka kuongezewa muda kiasi gani na sababu za kuongezwa muda. 

 

Vilevile kutokana na umuhimu wa mradi huo Waziri Ndumbaro amemuagiza Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Geophrey Pinda kukagua maendeleo ya ujenzi huo mara moja kila mwezi ili kuhakikisha ujenzi unaenda kwa kasi na kwa viwango.

 

Naye, Naibu Waziri Mhe. Geophrey Pinda alimtaka Mkandarasi kuongeza vibarua ili kazi iweze kukamilika kwa wakati na kama kuna changamoto za utekelezaji wa mradi basi zielezwe mapema ili kuona namna ya kuweza kuzitatua na zisikwamishe utekelezwaji wa mradi.

 

Awali akitoa taarifa ya utekelezaji wa mradi huo Mratibu wa Majengo ya Serikali Bw. Meshack Bandawe alisema kwa ujumla ujenzi unaendelea vizuri na ameipongeza Wizara ya Katiba na Sheria kwa kuwa ni moja ya Wizara zinazofanya vizuri katika ujenzi huo na amemsisitiza Mkandarasi kuongeza vifaa na vibarua ili kuweza kukamilisha kazi kwa wakati.


Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YAIPONGEZA WIZARA KWA UTEKELEZAJI WA MAMA SAMIA LEGAL AID CAMPAIGN

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA