WAZIRI NDUMBARO AZINDUA RASMI KIKOSI KAZI CHA ULINZI KWA WATOTO DHIDI YA BIASHARA YA USAFIRISHAJI HARAMU WA BINADAMU


 



XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX

Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Damas Ndumbaro amezindua rasmi kikosi kazi cha Ulinzi wa watoto dhidi ya biashara ya Usafirishaji haramu wa binadamu,  hafla hiyo ya uzinduzi imefanyika leo tarehe 21 Julai, 2022 Jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na wadau kutoka katika taasisi na sekta mbali mbali. 

 

 Dkt. Ndumbaro amesema Wizara ya Katiba na Sheria  ndiyo Wizara inayoshughulikia  haki za binadamu  hivyo siku ya leo ni siku muhimu Sana katika historia ya haki jinai. 

 

"Uhalifu huu ni mkubwa sana, ni uhalifu wa kupanga na wa kimataifa, na uko maeneo makubwa, umevuka mipaka, wanasafirisha watoto hususani wasichana." alisema Dkt. Ndumbaro.

 

Aidha, Waziri Ndumbaro amesema mradi huu ni wa miaka minne na kikosi kazi hiki kitajengewa uwezo kuhakikisha kinakabiliana na wahalifu  kwa vitendo na kwa kila namna, amesema jukumu la kikosi kazi hiki ni kuwashughulikia wahalifu  pamoja na kuhakikisha wahalifu wanaohusika, mkono wa Sheria unachukua nafasi yake. 

 

Dkt. Ndumbaro ameagiza kikosi kazi hicho kutoa ulinzi na uhifadhi kwa waathirika wa vitendo hivyo ikiwemo kutoa msaada wa kisaikolojia na elimu pamoja na kuwalinda watu wote wanaotoa ushahidi.

 

Pamoja na hayo, Dkt. Ndumbaro ametoa wito kwa Wakurugenzi wa Mashitaka Tanzania Bara na Zanzibar, kuhakikisha mradi huo unatekelezwa kwa asilimia mia moja, pamoja na  kufanya tathmini mara kwa mara kubaini wapi panatakiwa kufanyiwa marekebisho.

 

Naye Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima amesema Wizara yake itakuwa mstari wa mbele kupigania haki za watoto kwa kushirikiana na wadau mbalimbali.

 

Aidha uzinduzi huo umehudhuriwa na Wadau wa Maendeleo kutoka IOM, UNICEF, Ubalozi wa Uingereza, Umoja wa nchi za Ulaya pamoja na UNDP, ambao wamepongeza jitihada za Tanzania katika kupambana na uhalifu mkubwa wa kupangwa na wameahidi kuendelea kushirikiana na Serikali katika vita dhidi ya biashara ya usafirishaji haramu wa binadamu haswa watoto.


Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YAIPONGEZA WIZARA KWA UTEKELEZAJI WA MAMA SAMIA LEGAL AID CAMPAIGN

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA