MABORESHO YA SHERIA YA MSAADA WA KISHERIA
XXXXXXXXXX
Wataalam kutoka Wizara ya Katiba na Sheria wamekutana na
kuanza kujadili Sheria ya Huduma za Msaada wa Kisheria, ili kuainisha maeneo
yanayohitaji kuboreshwa.
Kikao kazi hicho kinaongozwa na Mkurugenzi wa
Huduma za Msaada wa Kisheria na Msajili wa huduma hizo, Bi. Felistas Mushi na
kinafanyika Jijini Dar es salaam kuanzia tarehe 09/08/2022 kwa ufadhili kutoka
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu-LHRC.
Comments
Post a Comment