NAIBU WAZIRI PINDA AKABIDHI VIFAA VYA KUENDESHEA MAHAKAMA MTANDAO
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Geophrey
Pinda amekabidhi vifaa mbali mbali vya kuendeshea Mahakama mtandao tarehe
18 Agosti, 2022 katika gereza la mahabusu Wilayani Mpanda.
Vifaa hivyo ambavyo ni Kompyuta mpakato
(Laptop) Luninga, Kamera na vingine, vitatumika kuendeshea Mahakama mtandao,
ili kuweza kutatua kesi mbalimbali pamoja na kupunguza idadi kubwa ya mahabusu
walioko katika gereza hilo.
Akiongea na maafisa wa gereza hilo pamoja na
viongozi mbalimbali wa Serikali Mhe. Pinda amesema dhamira ya Serikali ni
kuondoa mlundikano wa mahabusu katika Magereza zetu.
Aidha, Mhe. Pinda amemuagiza DPP wa Mkoa wa
Katavi ndugu Abel Mwandalama kuondoa kesi zisizo na mashiko Ili kuondoa mlundikano
wa mahabusu kwenye gereza hilo.
Mhe. Pinda amemuagiza DPP kuhakisha kesi
zinaendeshwa kwa weledi na kwa kuzingatia haki pamoja na kufanya upelelezi kwa
wakati.
Mheshimiwa Pinda amesema serikali imetenga
kiasi cha shilingi bilioni tisa kwa ajili ya kujenga Mahakama shirikishi
itakayojengwa hapa mpanda. Mahakama hiyo itajumuisha Mahakama ya Mwanzo,
Wilaya, Mkoa, Rufaa pamoja na Mahakama Kuu.
Comments
Post a Comment