NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA MHE. GEOPHREY PINDA AWATAKA WATOA HUDUMA ZA MSAADA WA KISHERIA KUTOKIUKA KANUNI


Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Geophrey Pinda akihutubia wadau wanaotoa huduma ya msaada wa kisheria kwa mkoa wa Ruvuma, leo tarehe 29 Julai 2022.


 

. Katibu Mkuu wa  Wizara ya Katiba na Sheria, Bibi. Mary Makondo akizungumza na watoa huduma ya msaada wa kisheria kwa mkoa wa Ruvuma kabla ya kumkaribisha Mgeni Rasmi, leo tarehe 29 Julai 2022.

 

Watendaji wa Wizara ya Katiba na Sheria pamoja na watendaji wa ofisi ya Mkoa wa Ruvuma katika picha na Mgeni Rasmi, Mhe. Geophrey Pinda, leo tarehe 29 Julai 2022. Ruvuma


XXXXXXXXXXXXXXXX 

Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Geophrey Pinda amewataka Watoa Huduma za Msaada wa Kisheria na Wasaidizi wao kutokiuka kanuni za Sheria ya Msaada wa Kisheria.

 

Mhe. Pinda ameyasema hayo leo tarehe 29 Julai, 2022 katika maadhimisho ya Tamasha la Majimaji ya Selebuka, linaloendelea kufanyika Wilayani Songea wakati akiongea na Watoa huduma ya Msaada wa Kisheria pamoja na Wasaidizi wa Kisheria. 

 

“mnatakiwa kuwa nuru na washauri wema wa kupinga dhuluma, unyanyasaji na vitendo vyote vya ukatili kupitia mifumo mbalimbali iliyopo kuanzia ngazi ya kijiji/mtaa hadi Taifa” alisema Mhe. Pinda.

 

Aidha, Naibu Waziri amesema Wizara inatambua mchango  mkubwa unaofanywa  na  Watoa Huduma ya Msaada wa Kisheria hapa nchini na itaendelea kuimarisha mashirikiano na wadau wote na kuboresha mazingira ya utoaji wa huduma ya msaada wa kisheria.

 

Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Bibi. Mary Makondo amewapongeza watoa huduma hao kwa kazi yao kwa jamii, na kusisitiza wasivunjike moyo wanapokutana na changamoto bali iwe chachu ya kufanya kazi zaidi katika kuwatumikia watanzania.


Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YAIPONGEZA WIZARA KWA UTEKELEZAJI WA MAMA SAMIA LEGAL AID CAMPAIGN

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA