WAZIRI NDUMBARO AFANYA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA CANADA
XXXXXXXXXXXXXX
Waziri wa Katiba na Sheria
Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Canada
nchini Mhe. Pamela O'Donnell ambaye amefika kumuaga akitarajia kumaliza muda
wake wa utumishi mwishoni mwa mwezi Agosti 2022.
Maeneo waliyozungumzia ni pamoja na
kubadilishana ujuzi katika ulinzi wa mali asilia, masuala ya haki za binadamu
hususani ulinzi kwa watoto, mchakato wa upatikanaji wa katiba mpya, mchakato wa
kurekebisha sheria ya ndoa na sheria zinazohusu ushiriki wa wanawake katika
siasa.
Comments
Post a Comment