WAZIRI NDUMBARO AZURU OFISI YA MASHTAKA NJOMBE
XXXXXXXXXXXXXXXX
Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Damas
Ndumbaro(Mb), ametembelea Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Mkoani Njombe akiwa
ameambatana na Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu tarehe 18 Agosti
2022.
Katika ziara hiyo Dkt. Ndumbaro amewaasa
watumishi kuendelea kufanya kazi kwa bidii na kwa uadilifu.
Aidha, Dkt. Ndumbaro ameainisha kuwa jitihada
zinaendelea ili kuiwezesha Ofisi hiyo kutatua changamoto mbalimbali
zinazoikabili kwa kuona namna ya kuongeza bajeti kwa mwaka wa fedha ujao na
kuendelea na mazungumzo na wadau mbalimbali.
Dkt. Ndumbaro amekutana pia na Mkuu wa Mkoa wa
Njombe Mhe. Antony Mtaka ambapo wamepata wasaa wa kuzungumza masuala mbalimbali
yahusuyo haki jinai na utoaji haki kwa ujumla
Comments
Post a Comment