WIZARA YA KATIBA NA SHERIA YAHUDUMIA WANANCHI ZAIDI YA 400 MAJIMAJI SELEBUKA 2022, 81 WAKIPATIWA HUDUMA YA MSAADA WA KISHERIA.

 


XXXXXXXXXXXXXXXXX


Wizara ya Katiba na Sheria imetoa huduma kwa wananchi zaidi ya 400 katika Tamasha la Majimaji Selebuka lililomalizika leo 30 Julai, 2022 wilayani Songea-Ruvuma.

 

Akifunga Tamasha hilo Mbunge wa Songea Mjini ambaye pia ni Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro ameipongeza Wizara ya Katiba na Sheria kwa kushiriki na kutoa huduma katika Tamasha hilo.

 

“Natoa pongezi kwa Wizara ya Katiba na Sheria kwa ushiriki wenu na huduma za msaada wa kisheria mliotoa kwa wananchi waliofika kuwatembelea" alisema Dkt. Ndumbaro.

 

Katika tamasha hili lililoanza tarehe 23 Julai, Wizara kwa kushirikiana na watoa huduma za msaada wa kisheria (paralegals) wametoa huduma za msaada wa kisheria kwa wananchi 81 wilayani Songea.

 

Aidha, nakala 270 za Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na vipeperushi mbalimbali vya sheria ya ndoa, mtoto, mirathi na ardhi vimegawiwa bure kwa wananchi waliotembelea banda la Wizara.

 


Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YAIPONGEZA WIZARA KWA UTEKELEZAJI WA MAMA SAMIA LEGAL AID CAMPAIGN

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA