ZAIDI YA WANANCHI 200 WAPATA ELIMU YA MASUALA YA SHERIA KWENYE MAONESHO YA NANENANE MBEYA.


 

XXXXXXXXXXXXXXXXXXX


Mamia ya wahudhuriaji wamefurahishwa na Banda la Wizara ya Katiba na Sheria kwenye maonesho ya Nanenane yanayoendelea kwenye Viwanja vya John Mwakangale jijini Mbeya.

 

Maonesho ya Nanenane Mwaka huu yamebeba kauli mbiu isemayo; agenda 10/30 Kilimo ni biashara; jiandae kuhesabiwa kwa Mipango bora ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi. 

 

Wananchi mbalimbali waliohudhuria kwenye Banda la Wizara ya Katiba na Sheria wamepata wasaa wa kujifunza na kuuliza maswali mbalimbali hasa kuhusu sheria ya ndoa, ya ardhi, mirathi na sheria ya mtoto.

 

Zaidi ya wananchi 200 wamepatiwa elimu na ushauri wa Kisheria.

 

Aidha, suala la mirathi ndio limekuwa likiulizwa Kwa wingi na wananchi kupatiwa ufafanuzi na maelekezo ya kuweza kutatua tatizo hilo.

 

Maonesho haya yamefungwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo Agosti, 08, 2022.

 


Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YAIPONGEZA WIZARA KWA UTEKELEZAJI WA MAMA SAMIA LEGAL AID CAMPAIGN

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA