DKT. KAZUNGU AWATAKA WADAU WA MAZINGIRA WASHIRIKI KATIKA UPANDAJI NA UTUNZAJI WA MITI KATIKA MAZINGIRA WALIYOPO
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Dkt. Khatibu Kazungu akipanda mti katika zoezi la upandaji miti katika Maadhimisho ya Miaka 20 ya Kuanzishwa kwa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora.Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Dkt. Khatibu Kazungu akiongoza maandamano katika zoezi la upandaji miti katika Maadhimisho ya Miaka 20 ya Kuanzishwa kwa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora.Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Dkt. Khatibu Kazungu akizungumza katika zoezi la upandaji miti katika Maadhimisho ya Miaka 20 ya Kuanzishwa kwa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora.
Naibu Katibu Mkuu wa
Wizara ya Katiba na Sheria Dkt. Khatibu Kazungu amewataka wadau wote wa
Mazingira kushiriki katika upandaji na utunzaji wa miti katika mazingira
waliyopo ili kutekeleza Mkakati wa Utekelezwaji wa Sera ya Taifa ya Uhifadhi wa
Mazingira wa mwaka 2020/21.
Dkt. Kazungu ameyasema hayo wakati wa tukio la upandaji miti
ikiwa ni mojawapo ya shughuli za Maadhimisho ya Miaka Ishirini tangu kuanzishwa
kwa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora lililofanyika leo, Septemba 10, 2022
eneo la kwa Swai Nkuhungu, jijini Dodoma.
Dkt. Kazungu alisema moja ya changamoto za uhifadhi wa
mazingira nchini ni ukataji miti na uharibifu wa misitu.
‘’Taarifa ya tatu ya mazingira nchini ya mwaka 2019 inaonesha
kuwa takriban hekta 469,420 za misitu kwa mwaka hupotea kutokana na utegemezi
mkubwa wa nishati ya kuni na mkaa kwa ajili ya kupikia, kilimo na ufugaji wa
kuhamahama’’ alisema Dkt. Kazungu.
Dkt. Kazungu aliongeza kuwa ‘’ inakadiriwa kuwa ili kurejesha
eneo la misitu linalopotea kila mwaka inahitajika kupanda na kutunza miti
katika eneo lenye ukubwa wa hekta 185,000 sawa na miti 2,280,000 kwa mwaka kwa
muda wa miaka 17 mfululizo’’
Aidha, Dkt. Kazungu amesema Serikali imeandaa Mkakati wa
Utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Uhifadhi wa Mazingira kwa kipindi cha kuanzia mwaka
2021 hadi 2032.
Awali akimkaribisha mgeni rasmi, Mwenyekiti wa Tume ya Haki
za Binadamu na Utawala Bora Jaji mstaafu Mhe. Mathew Maimu amesema utekelezaji
wa haki za binadamu ni muhimu kwa
mazingira salama ili kuwezesha jamii kuishi mahali pa utulivu na usalama na
kuwezesha kufanya shughuli zao za kiuchumi kwa maendeleo ya nchi.
Naye, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mhe. Jabir Shekimweri ameipongeza
Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora kwa zoezi la upandaji miti na kuwasihi
kuwa katika maadhimisho hayo ya kutimiza miaka 20 wajitahidi kutatua
changamoto za wananchi wa Dodoma hasa
kwenye sekta ya ardhi na mirathi.
Katika zoezi hilo la upandaji miti Miche 600 ya matunda na
kivuli imepandwa katika eneo la ekari mbili.
Kauli mbiu ya Maadhimisho hayo ni ‘’Miaka 20 ya Kuhamasisha Ulinzi na Hifadhi ya Haki za Binadamu na
Utawala Bora kwa Maendeleo ya Nchi’’.
Comments
Post a Comment