NAIBU WAZIRI PINDA AWATAKA WATUMISHI KUZINGATIA SHERIA ZA UTUMISHI WA UMMA

Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Geophrey Pinda akizungumza na Menejimenti ya RITA.
 
Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Bi. Mary Makondo akizungumza na Menejimenti ya RITA.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Dkt. Khatib kazungu akizungumza na Menejimenti ya RITA.

Picha ya pamoja.
XXXXXXXXXXXXX


Naibu waziri Mhe. Geophrey Mizengo Pinda amewataka watumishi kuheshimu na kuzingatia Sheria za utumishi wa Umma sambamba na kuheshimiana kila mmoja wakati wa utekelezaji wa majukumu ya kila siku.

 

# Ameyasema hayo leo tarehe 6 Septemba, 2022 Jijini Arusha wakati akizungumza na Menejimenti ya RITA katika kikao kazi Cha kuwajengea uelewa katika kuzingatia kanuni, miongozo ya utumishi wa Umma ili Kuunga mkono jitihada za Serikali za kiwaletea Maendeleo wananchi. 

 

#Mhe. Pinda ameongeza kuwa Menejimenti inatakiwa kuwa makini katika kufanya maamuzi na kufuata misingi ya Sheria, uadilifu na busara hasa itakapotokea mtumishi amekwenda kinyume na kutakiwa kuchukuliwa hatua za kinidhamu.

 

# Pia ameagiza kila kiongozi kukubali mabadiliko ya uongozi kuanzia ngazi ya Serikali kuu, Wizara na ndani ya Taasisi ili kwa pamoja Kuunga mmono na kutekeleza maelekezo ya Serikali iliyopo madarakani kwa Sasa.

 

#Kuhusu uvujishaji wa Siri ya vikao vya ndani wakati wa kufanya maamuzi Mhe. Pinda amesema katika utendaji wa Serikali tabia hiyo ni sumu mbaya na haikubaliki kwani inasababisha migogoro na kushindwa kuchukuliwa hatua za kinidhamu kwa wakati kwa baadhi ya watumishi wasiyotekeleza majukumu yao ipasavyo.

 

#Mhe. Pinda amesisitiza mnyororo wa Mawasiliano baina ya Taasisi zilizopo chini ya Wizara ya Katiba na Sheria kwani ndiyo chombo pekee cha kuzitetea na  kuziwakilisha katika vikao vya juu vya maamuzi ikiwemo makadirio ya bajeti ya Wizara na Taasisi zake.

 

" Wizara tunawajibika kwa Serikali kutoa taarifa  ya utekelezaji wa kila Taasisi iliyopo chini ya Wizara hii hivyo ni muhimu Menejimenti zote kutambua wajibu wenu Kwetu kama viongozi wenu wa kuwasemea katika vikao  vya maamuzi vya Kitaifa".Alisema Mhe.Pinda.

 

# Mhe. Pinda amewapongeza Wafanyakazi na Menejimenti ya RITA kwa kushirikiana vizuri na Wizara katika utekelezaji wa mikakati mbalimbali ikiwemo ya Usajili wa watoto wa umri chini ya miaka mitano katika Mikoa 26 ya Tanzania Bara ambapo watoto zaidi ya 7.5 wamesajiliwa na kupatiwa vyeti vya Kuzaliwa bila ya malipo.

 

# Naye Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Bi. Mary Makondo amesema Wizara inapokea na kufanyia kazi mahitaji ya kila Taasisi hivyo RITA isisite kuwasilisha mahitaji kwa wakati.

 

# Kwa upande wake Kabidhi Wasii Mkuu na Afisa Mtendaji Mkuu wa RITA Bi. Angela Anatory amesema kikao hicho kinafanyika wakati muafaka kutokana na mabadiliko ya uongozi yaliyofanyika ili kwa pamoja kushirikiana kuboresha na kubuni upya mikakati itakayosaidia kufikia malengo ya kutoa huduma bora kwa Wananchi.

 

# Aidha ameishukuru Wizara kwa kukubali kufanyika Kwa kikao kazi hicho hivyo kuahidi kupokea na kutekeleza maelekezo na ushauri wa viongozi Wakuu wa Kitaifa chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan.

 

"Mhe. Naibu Waziri tunakuahidi kama Menejimenti tutashirikiana na Wizara yako kuhakikisha tunatekeleza maagizo yote na tutawajibika ipasavyo ili RITA isonge mbele". Alisema Bi. Anatory.

 

# Kikao kati ya Wizara ya Katiba na Sheria na Menejimenti ya RITA kitaendelea Kwa siku tatu na kutatolewa mafunzo maalum ya uongozi, Sheria na miongozo ya utumishi wa Umma.

 


Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YAIPONGEZA WIZARA KWA UTEKELEZAJI WA MAMA SAMIA LEGAL AID CAMPAIGN

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA