WAZIRI NDUMBARO AZINDUA KAMPENI YA UTOAJI WA HUDUMA ZA MSAADA WA KISHERIA
Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Damas Ndumbaro
amezindua kampeni ya utoaji wa huduma za msaada wa Kisheria tarehe
8 Septemba 2022, Jijini Arusha.
Wakati akizungumza na Wananchi wa Kata
ya Ikiding'a, Halmashauri ya Wilaya ya Arusha, Dkt. Ndumbaro amesema Utoaji wa
hudumu za msaada wa kisheria utamsaidia mwananchi mnyonge kupata huduma za
Mawakili pasipo na malipo.
"Serikali inatambua kuwa siyo kila
mwanachi ana uwezo wa kulipia gharama za kisheria, hivyo katika huduma hii tuna
wadau mbali mbali ambao tunashirikiana nao kama vile TLS, TAWLA, Asasi za
kiraia, pamoja na wadau wengine". alisema Dkt. Ndumbaro
Aidha, Dkt. Ndumbaro ameshiriki pia kutoa
huduma za msaada wa kisheria kwa kuhudumia wananchi mbali mbali kama
Wakili.
Uzinduzi huo ulihudhuriwa pia na Naibu
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Geophrey Pinda, Katibu Mkuu Bi. Mary Makondo
pamoja na Naibu Katibu Mkuu Dkt. Khatibu Kazungu.
Comments
Post a Comment