IDARA NA SEKTA ZINAZOHUSIKA NA UTAJIRI ASILI NA MALIASILIA ZIFANYE KAZI KWA PAMOJA: BI. MAKONDO


 


XXXXXXXXXXXXXXXXX

Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Bi. Mary Makondo amezitaka Idara na Sekta za Serikali zinazohusika na usimamizi wa Utajiri Asili na Maliasilia za Nchi kufanya kazi kwa pamoja kuhakikisha wananchi wananufaika na utajiri asilia na maliasilia za nchi. 

 

Bi. Makondo ameyasema hayo wakati akifungua kikao kazi cha kujadili utekelezaji wa Mpango wa Kusimamia Utajiri Asili na Maliasilia za Nchi (Natural Wealth and Resources Socio-Economic Governance Programme) leo tarehe 6 Oktoba, 2022 Jijini Arusha.

 

“Najua mnawakilisha ofisi zenu, mnawakilisha Wizara zenu lakini tukumbuke tu wamoja, tunajenga Tanzania moja hivyo tufanye kazi kwa pamoja kuhakikisha mpango huu haupunguzi tu  umaskini kwa Watanzania bali pia unaongeza Pato la Taifa.” Alisema Bi Makondo.

 

Mradi huo unatekelezwa na Wizara ya Katiba na Sheria kwa ufadhili wa Serikali na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP).

 

Kikao hicho kimehudhuriwa pia na Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt. Zainabu Chaula, Wadau kutoka Sekta na Idara za Serikali zinazoshughulika na  Utajiri Asili na Maliasilia za Nchi pamoja na baadhi ya Wabia wa Maendeleo kutoka UNDP. 

 

Akitoa salaam zake, Dkt. Chaula amekumbusha washiriki kwamba wana jukumu la kumsaidia Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupunguza changamoto za Watanzania hivyo anayo matumaini makubwa kwamba mradi utafika mwisho na kutimiza malengo yake mazuri ya kutatua changamoto za wananchi. 

 

Naye ndugu Amon Manyama kutoka UNDP amesema mradi huo ni mzuri unategemewa kunufaisha Watanzania kiuchumi, amesisitiza ushirikishwaji wa wanawake, vijana na jamii ya chini kabisa ambako ndiko kuliko na wananchi wengi.


Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YAIPONGEZA WIZARA KWA UTEKELEZAJI WA MAMA SAMIA LEGAL AID CAMPAIGN

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA