KIKAO CHA WADAU KAMATI YA TATHMINI YA MRADI WA ACCESS TO JUSTICE AND RULE OF LAW
XXXXXXXXXXXXXX
Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Bi.
Mary Makondo ameshiriki kikao cha Wadau Kamati ya Tathmini ya Mradi wa Access
to Justice and Rule of Law (Local Project Appraisal Comittee) unaofadhiliwa na
UNDP. Kikao hicho kilifanyika tarehe 4 Oktoba, 2022 Jijini Dar es Salaam.
Kikao kilipitia andiko la mradi na kutoa
mapendekezo ya kuanza utekelezaji wake. Mradi huo ni wa miaka mitatu 2022/23 -
2024/25, na ni mwendelezo wa mradi wa Access to Justice and Human Rights
Protection ulioisha mwaka 2021.
Mradi utatekelezwa na Wizara ya Katiba na
Sheria kwa kushirikiana na Ofisi ya Taifa ya Mashtaka - NPS, Tume ya Haki za
Binadamu na Utawala Bora - CHRAGG, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu, Magereza na
Polisi.
Comments
Post a Comment