WIZARA YA KATIBA KUTOA HUDUMA ZA KISHERIA KIDIJITALI – DKT NDUMBARO
Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Damas Ndumbaro akifungua warsha ya siku mbili kwa watoa Huduma za Msaada wa Kisheria.Washiriki wakiendelea na pamoja.Picha ya pamoja.
Waziri
wa Katiba na Sheria Dkt. Damas Ndumbaro amesema Wizara ya Katiba na Sheria
imekusudia kuhakikisha huduma za kisheria zinazotolewa na Wizara na Taasisi
zilizo chini yake zinapatikana kwa njia ya TEHAMA.
Dkt.
Ndumbaro ameyasema hayo wakati akifungua warsha ya siku mbili kwa Wasajili
Wasaidizi wa Watoa Huduma za Msaada wa Kisheria, Wasaidizi wa Kisheria,
Mawakili, Wanasheria na Maafisa wa Jeshi la Magereza ambayo inafanyika kuanzia
leo Oktoba 17, 2022 Jijini Arusha.
Dkt
Ndumbaro amesema “Kwa kutambua umuhimu wa TEHAMA kwenye utoaji wa huduma,
Wizara ya Katiba na Sheria imekusudia kuhakikisha huduma za kisheria
zinazotolewa na Wizara na Taasisi zilizo chini yake zinapatikana kwa njia ya
TEHAMA. Hili litawezesha huduma kupatikana kwa wakati na hatimaye kuwezesha
vyombo vingine vya utoaji haki kutoa haki kwa wakati na kwa gharama nafuu.”
Dkt.
Ndumbaro ameongeza kuwa TEHAMA imekuwa na mchango mkubwa kwenye utoaji wa
huduma na utendaji wa Serikali kwa ujumla. Faida zinazopatikana ni pamoja
na kuwepo kwa utunzaji wa kumbukumbu
sahihi za wananchi, kuweka uwazi na
uwajibikaji wa utoaji huduma hususan panapokuwa na malalamiko kutoka kwa
wananchi, kurahisisha upatikanaji wa huduma, na vilevile kuondoa mianya ya
rushwa kwenye utoaji huduma kwa kuwa
hakuna mwingiliano kati ya mtoa huduma na mteja.
Dkt.
Ndumbaro alisisitiza kuwa ni vyema kuwa na mifumo mizuri ya kisheria ambayo
itarahisisha upatikanaji wa haki kwa wakati; mifumo ambayo itawezesha wananchi
kupata huduma za kisheria popote walipo kwa gharama nafuu katika kuifikia haki.
Uwepo wa mifumo, utawapunguzia wananchi muda na gharama za kushughulikia
masuala ya kisheria na badala yake watajikita zaidi katika shughuli zingine za
kiuchumi na kimaendeleo hivyo basi kuleta maendeleo ya mtu mmoja mmoja na Taifa
kwa ujumla.
Aidha,
Dkt. Ndumbaro aliongeza kuwa Wizara ina jukumu kubwa la kutoa elimu ya
Katiba na Sheria kwa wananchi hususan
vijana kwani hiyo itawasaidia kujua sheria na kudai haki zao.
Dkt.
Ndumbaro amesema “Naamini kwamba Wizara ina jukumu kubwa la kutoa elimu ya
Katiba kwani huwezi kwenda kutoa kitu kipya wakati hujui cha zamani, tupate
elimu ya Katiba iliyopo sasa ili tujue mazuri yakwenda nayo katika Katiba mpya
na kuacha mabaya yaliyopo.”
Akimkaribisha
Waziri Ndumbaro kufungua warsha hiyo, Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa Bw. David
Lyamongi amesema Wasaidizi wa kisheria wapewe kipaumbele katika kutekeleza kazi
zao kwani wanasaidia sana jamii hasa wajane na yatima.
Bw.
Lyamongi amesema “mchango wa Wasaidizi wa Kisheria ni mkubwa sana katika jamii
hususan katika Mkoa wa Arusha kwenye masuala ya kisheria yaliyomshinda
mwananchi au kushindwa kwenda mwenyewe mahakamani hivyo kuhitaji uwakilishi.”
Msajili
wa Watoa Huduma za Msaada wa Kisheria nchini Bi. Felistas Mushi amesema mafunzo
hayo yamewashirikisha Watoa Huduma za kisheria kutoka kwenye Mashirika kumi na
tano, Wasajili Wasaidizi na Maafisa Magereza kutoka mikoa kumi ya Tanzania
Bara. Washiriki hao wamechaguliwa kwa sababu wapo karibu na wananchi sanjali na
kuwasaidia wananchi wengi wa chini waliopo kwenye maeneo yao.
Awali
akitoa maelezo ya utangulizi Mkuu wa Kitengo cha TEHAMA Bw. Gabriel Ally
amesema mafunzo hayo yatafanyika kwa awamu nne kwa mwaka wa fedha 2022/2023.
Bw.
Gabriel amesema huduma za TEHAMA zinarahisisha kufikisha huduma za kisheria kwa
wananchi popote pale walipo hivyo ni muhimu makundi hayo manne yakazingatia
mafunzo hayo katika utendaji kazi wao kwa kuwa zinahusiana na wananchi kwa
kiasi kikubwa.
Mafunzo
haya yanahusisha mifumo inayohusu usajili wa watoa huduma za msaada wa kisheria
na wasaidizi wa kisheria ambazo zinatolewa chini ya Sheria ya Msaada wa
Kisheria ya Mwaka 2017, mfumo wa usajili wa watoa huduma za maridhiano,
usuluhishi, na upatanishi kama ilivyobainishwa chini ya Sheria ya Usuluhishi ya
Mwaka 2020. Mifumo mingine ni pamoja na
uwasilishaji wa malalamiko, maombi ya huduma za msaada wa kisheria, maombi ya
kuongezewa muda wa kuwasilisha mashauri mahakamani nje ya muda pamoja na huduma
nyingine za kisheria.
Comments
Post a Comment