JIUNGENI NA CHAMA CHA MAWAKILI CHA AFRIKA MASHARIKI- MHESHIMIWA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN
Rais Samia Suluhu Hassan amewataka Mawakili nchini kujiunga na Chama Cha Mawakili Cha Afrika Mashariki (East Africa Law Society).
Mheshimiwa Rais ameyasema hayo wakati akifungua mkutano wa siku tatu wa Chama Cha Mawakili Cha Afrika Mashariki tarehe 24 Novemba, 2022 Jijini Arusha .
Akiongea kwenye kikao hicho Mhe. Rais amesema "Afrika Mashariki Sasa ni wamoja tunafanya kazi kwa kushirikiana, na nyinyi shirikianeni kutatua kesi mbalimbali ndani ya Jumuiya yetu na nje ya Jumuiya, kuweni wamoja na imara katika kujenga Chama chenu"
Aidha Mheshimiwa Rais amewaomba Mawakili kuwakaribisha Mawakili kutoka DRC Congo , ambao wamejiunga na Jumuiya ya Afrika Mashariki hivi karibuni.
Naye Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Geophrey Pinda ambaye alimwakilisha Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro amesema " ni fursa kwa Mawakili wetu kufanya kazi ndani ya Afrika Mashariki kwasababu watajijengea uwezo na kujifunza mambo mengi kutoka kwa wengine, nafasi kama hizi zinakufanya ujue mambo mbalimbali ya kisheria pamoja kutambulika kimataifa".
Pia Mhe. Pindaa amewataka Mawakili wa Chama hicho kushirikiana katika kutatua kesi mbalimbali.
Comments
Post a Comment