JUKUMU LA KUHIFADHI WAKIMBIZI SIYO JEPESI HASA KWA NCHI WENYEJI- MHE PINDA


Naibu Waziri wa Katiba na Sheria  Mhe. Geophrey  Pinda  akifunga kikao kazi cha siku tatu cha kujadili masuala mbalimbali ya Wakimbizi na Wahamiaji kilichofanyika jijini, Arusha.
Washiriki wa kikao.

Picha ya pamoja.
XXXXXXXXXXXXXXXXXX

Naibu Waziri wa Katiba na Sheria  Mhe. Geophrey  Pinda amesema  kipindi hiki ambacho dunia inakabiliwa na  changamoto  ya kuwa na idadi kubwa ya watu wanaokimbia makazi yao  jukumu la kuhifadhi Wakimbizi ni jukumu zito hasa kwa nchi inayopokea Wakimbizi. 

Mhe. Pinda ameyasema hayo  wakati akifunga kikao kazi cha siku tatu cha kujadili masuala mbalimbali ya Wakimbizi na Wahamiaji kilichofanyika  kuanzia tarehe 16 hadi 18 Novemba, 2022 jijini Arusha.

Katika kikao hicho Mhe. Pinda amesema " Serikali imekuwa ikihifadhi Wakimbizi kwa muda mrefu, hivyo inatambua mchango mkubwa wa wadau wa masuala ya Wakimbizi katika nyanja zote".

Aidha, Mhe. Pinda amesema "kama mnavyofahamu  Wakimbizi wengi  wanahifadhiwa katika nchi zinazoendelea na Tanzania tuna Wakimbizi  zaidi ya  256,000 ambao wamehifadhiwa kwenye kambi mbali mbali nchini".
 
Naye Mkurugenzi  wa Idara ya Huduma Kwa Wakimbizi kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi ndugu, Sudi Mwakibasi  amesema Serikali imekuwa ikitoa ushirikiano mzuri na wadau mbalimbali katika kuhudumia Wakimbizi na hii ni kwasababu tuna historia nzuri ya kupokea Wakimbizi kutoka nchi mbalimbali na wanaishi kwa amani na utulivu.

Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YAIPONGEZA WIZARA KWA UTEKELEZAJI WA MAMA SAMIA LEGAL AID CAMPAIGN

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA