WIZARA YA KATIBA NA SHERIA KUANDAA MPANGO KAZI WA UFUATILIAJI NA TATHIMINI.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Sera, Mipango, Ufuatiliaji na Tathmini ndugu Emmanuel Mayeji kwenye kikao kazi cha siku tano kinachofanyika kuanzia tarehe 28 Novemba hadi 2 Desemba 2022 mjini Morogoro.
Ndugu Mayeji amesema " kakao hiki kina malengo makuu mawili , Moja kujadili namna ya kuwa na mfumo thabiti wa Ufuatiliaji na Tathmini ya Utekelezaji wa Sera, Sheria na Kanuni , Miongozo na Mipango inayosimamiwa"
Mbili kuwa na mfumo thabiti wa utoaji wa taarifa za utekelezaji wa majukumu ya Wizara kwa kuzingatia takwimu sahihi za mafanikio na changamoto zilizojitokeza pamoja na kuwa na mkakati wa kutatua changamoto zilizojitikeza wakati wa utekelezaji" .
Aidha kikao kazi hicho kinahudhuriwa na maafisa mbalimbali kutoka Wizara ya Katiba na Sheria.
Comments
Post a Comment