DKT. DAMAS DUMBARO AZINDUA MAADHIMISHO YA SIKU YA MAADILI NA HAKI ZA BINADAMU


 

XXXXXXXXXXXXX

Waziri wa Katiba na Sheria Dkt.  Damas Ndumbaro amezindua maadhimisho ya siku ya Maadili na Haki za Bindamu kitaifa. 

Maadhimisho hayo yamezinduliwa  tarehe 6 Desemba, 2022 katika viwanja vya Nyerere Square vilivyopo katikati ya mji,  jijini Dodoma. 

Akiongea kwenye  Uzinduzi   huo Mhe. Dkt. Ndumbaro amesema "Maadhimisho haya yameanza mwaka 2016  kwa lengo la kuwa na siku ya kimataifa ya kupambana na Rushwa pamoja na siku ya kimataifa ya Haki za Binadamu  ili kuwaelimisha wananchi namna ya kupiga vita rushwa  na  pia  juu ya masuala ya Haki za Binadamu."

Pia Dkt. Ndumbaro amesema "Jukumu kubwa la Serikali yetu ni kuwaletea Wananchi  maendeleo, hivyo Usimamizi wa Maadili, Haki za Binadamu, Uwajibikaji, Uwazi na mapambano dhidi ya rushwa  ni masuala endelevu kwa kuwa ni msingi wa utoaji huduma bora kwa Umma."

Kauli mbiu ya maadhimisho hayo inasema _"Maadili, Haki za Binadamu, Utawala Bora na Mapambano dhidi ya Rushwa ni jukumu la pamoja kati ya Serikali, Wananchi na Wadau Wengine"._

Aidha, Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Bi. Neema Mwakalyelye amesema "kupiga vita Rushwa ni jukumu letu sote, rushwa inarudisha maendeleo nyuma."

Naye Mkurugenzi wa Idara ya Haki za Bindamu  Bi. Nkasori Sarakikya ambaye amemwakilisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria amesema "Wizara imejipanga kutoa elimu na Huduma Kwa Umma  kuhusu Haki za Binadamu na  Huduma ya Msaada wa Kisheria."

 


Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YAIPONGEZA WIZARA KWA UTEKELEZAJI WA MAMA SAMIA LEGAL AID CAMPAIGN

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA