Posts

Showing posts from 2023

UJENZI WA JENGO LA WIZARA WAFIKIA ASILIMIA 80

Image
  Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Dkt. Khatibu Kazungu akiongea kwenye kikao na Mkandarasi wa jengo la Wizara kabla ya kutembelea na kukagua jengo hilo, tarehe 29 Desemba, 2023 Mji wa Serikali Mtumba. 0   Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Dkt. Khatibu Kazungu akitembelea na kukagua ujenzi wa jengo la Wizara, tarehe 29 Desemba, 2023 Mji wa Serikali Mtumba. Mkandarasi Nasiri Nassoro akifafanua jambo wakati akitoa maelezo ya maendeleo ya ujenzi kwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Dkt. Khatibu Kazungu alipotembelea na kukagua ujenzi huo, tarehe 29 Desemba, 2023 Mji wa Serikali Mtumba 01  Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Dkt. Khatibu Kazungu akishauri jambo alipotembelea na kukagua ujenzi wa jengo la Wizara, tarehe 29 Desemba, 2023 Mji wa Serikali Mtumba. XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Na William Mabusi -   WKS Dodoma Ujenzi wa jengo la Wizara ya Katiba na Sheria linalojengwa Mji wa Serikali Mtumba limefikia asilimia themanini (80).

DKT. CHANA ATAKA WATUMISHI KUFANYA KAZI KWA KUZINGATIA MASLAHI YA TAIFA

Image
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana kwenye picha ya pamoja na Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya RITA, 22 Desemba, 2023 Jijini Arusha. Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akihutubia wakati akifungua kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya RITA, 22 Desemba, 2023 Jijini Arusha. XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Na William Mabusi – WKS Dodoma Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana ametoa wito kwa watumishi wa umma kufanya kazi kwa weledi na uadilifu kwa kuzingata maslahi mapana ya Serikali na Taifa kwa ujumla. Dkt. Chana ameyasema hayo wakati akifungua kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa ofisi ya RITA tarehe 22 Desemba, 2023 linalofanyika Jijini Arusha. Baraza hilo linafanyika ikiwa ni utekelezaji wa Sheria ya ajira na Mahusiano kazini. Amesema, “huduma ya usajili wa matukio muhimu ya binadamu na Takwimu mnazotoa ni huduma zinazowagusa wananchi moja kwa moja. Hivyo, mkiwa wafanyakazi mlioaminiwa na Serikali ya Tanzania endele

DKT. CHANA APOKEA CHETI CHA HESHIMA KUTOKA TAASISI YA KUPINGA RUSHWA

Image
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt Pindi Chana atunukiwa tuzo kutoka kwenye Taasisi ya Anti Corruptions Voices Foundations kwenye kilele cha Maadhimisho ya siku ya Maadili na Haki za Binadamu tarehe 10 Desemba, 2023 Jijini Dodoma. XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana amepokea cheti cha heshima kutoka Taasisi ya Kupinga Rushwa (Anti Corruptions Voices Foundations) alichotunukiwa kutokana na kuwa Mgeni Rasmi katika mbio za “Sepesha Rushwa Marathon.” Balozi Chana amekabidhiwa cheti hicho tarehe 10 Desemba, 2023 wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya Maadili na   Haki za Binadamu.

Wananchi watakiwa kuunga mkono jitihada za Serikali kupinga ukiukwaji wa haki za binadamu

Image
  Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiwa katika banda la Wizara ya Katiba na Sheria kwenye Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Maadili na Haki za Binadamu yaliyofanyika leo tarehe 10 Desemba 2023 Jijini Dodoma.  Mgeni rasmi Mhe. Kassim Majaliwa akiwa na viongozi wengine meza kuu kwenye kilele cha maadhimisho ya siku ya Maadili na Haki za Binadamu  yalifanyika leo tarehe 10 Desemba 2023 jijini Dodoma. Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akitoa hotuba kwenye Kilele cha Maadhimisho ya siku ya Maadili na Haki za Binadamu yaliyofanyika leo tarehe 10 Desemba 2023 Jijini Dodoma. Watumishi kutoka Wizara na Taasisi mbalimbali wakimsikiliza Mhe. Waziri Mkuu Kass im Majaliwa alipokuwa akihutubia kwenye kilele cha Maadhimisho ya siku ya Maadili na Haki za Binadamu yaliyofanyika leo tarehe 10 Desemba 2023 Jijini Dodoma. Waziri wa Katiba na Sheria Mhe Balozi Pindi Chana akitoa neon la utambulisho kwenye Kilele cha Maadhimisho ya siku ya Maadili na Haki za Binadamu yaliyofanyika leo tarehe 10 Desemba 2023 Jiji

TANZANIA IMESAJILI NA KUTOA VYETI VYA KUZALIWA KWA WATOTO ZAIDI YA MILIONI NANE

Image
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akihutubia wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mpango wa Usajili wa Watoto wa Umri chini ya miaka mitano, Desemba 08, 2023 katika viwanja vya Mbagala Zakhiem Jijini Dar es Salaam. Katibu Mkuu Wizira ya Katiba na Sheria Bi. Mary Makondo akihutubia wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mpango wa Usajili wa Watoto wa Umri chini ya miaka mitano, Desemba 08, 2023 katika viwanja vya Mbagala Zakhiem Jijini Dar es Salaam. Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akizindua Mpango wa Usajili wa Watoto wa Umri chini ya miaka mitano, Desemba 08, 2023 katika viwanja vya Mbagala Zakhiem Jijini Dar es Salaam. XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Na Lusajo Mwakabuku - DSM Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana amesema kuwa Watoto zaidi ya milioni 8.8 wamesajiliwa na kupatiwa vyeti vya kuzaliwa katika mikoa 26 ya Tanzania Bara kupitia Mpango wa Usajili wa Watoto wa Umri chini ya miaka mitano. Mhe. Waziri Balozi Dkt. Pindi Chana a

“UNYANYASAJI WA KIJINSIA HAUNA NAFASI KATIKA NCHI YETU” DKT. CHANA

Image
  Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akihutubia wakati akifungua Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia, tarehe 06 Desemba, 2023 Jijini Dodoma. Washiriki siku ya kufungua Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia, wakimkaribisha ukumbini Mgeni Rasmi Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana tarehe 06 Desemba, 2023 Jijini Dodoma. Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana kwenye picha ya pamoja na baadhi ya viongozi walioshiriki hafla ya kufungua Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia, tarehe 06 Desemba, 2023 Jijini Dodoma.                                    XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Na William Mabusi – WKS Dodoma Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana (Mb) amesema Tanzania inaweza kusonga mbele na kushinda vita dhidi ya Ukatili wa Kijinsia ikiwa wote tutazungumza na kupaza sauti kupinga Unyanyasaji wa kijinsia huku akiitaka jamii kushiriki kikamilifu katika kutoa ushahidi wa matukio ya unyanyasaji wa kijinsia mara inapo

NCHI IKITAWALIWA NA RUSHWA HAIWEZI KUFIKIA MALENGO: BI. MAKONDO

Image
  Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Bi. Mary Makondo akihutubia kwenye Jukwaa la Kitaifa la Wadau wa juhudi dhidi ya rushwa, tarehe 04 Desemba, 2023 Jijini Dodoma. Washiriki kwenye Jukwaa la Kitaifa la Wadau wa juhudi dhidi ya rushwa, wakisikiliza hotuba, tarehe 04 Desemba, 2023 Jijini Dodoma. Meza Kuu kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Watumishi wa Serikali kwenye Jukwaa la Kitaifa la Wadau wa juhudi dhidi ya rushwa, wakisikiliza hotuba, tarehe 04 Desemba, 2023 Jijini Dodoma. XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Na William Mabusi – WKS Dodoma Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Bi. Mary Makondo amezitaka Taasisi za Serikali na Sekta Binafsi kuweka mazingira ya kuzuia rushwa, kuepuka na kutokomeza vitendo vya rushwa nchini ili kuliwezesha taifa kufikia malengo mbalimbali iliyojiwekea katika kuleta maendeleo nchini. Bi. Makondo ameyasema hayo alipokuwa akihutubia kwenye Jukwaa la Kitaifa la Wadau wa juhudi dhidi ya rushwa tarehe 04 Desemba, 2023 Jijini Dodoma lililo hudhuriwa n

KUPIGA VITA RUSHWA NI JUKUMU LETU SOTE – MHE. PINDI CHANA.

Image
    Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Pindi Chana akiongea na Wananchi kwenye  Uzinduzi wa Maadhimisho ya   ya siku ya Maadili  na Haki za Binadamu  Kitaifa yalifanyika uwanja wa Jamhuri leo tarehe 03 Desemba 2023  Jijini Dodoma Waziri wa katiba na sheria Mhe. Pindi Chana akiwa na viongozi  meza kuu  kwenye Uzinduzi wa Maadhimisho ya   ya siku ya Maadili  na Haki za Binadamu  Kitaifa yalifanyika uwanja wa Jamhuri leo tarehe 03 Desemba 2023  Jijini Dodoma  Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Pindi Chana akiwa katika picha ya pamoja na mshindi wa mbio za Sepesha Rushwa Marathoni   kilomita 21  kwa upande wa wanawake leo tarehe 03 Desemba  2023 Jijini Dodoma.  XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Na George Mwakyembe – WKS Dodoma.   Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana amesema kuwa uwepo wa vitendo vya rushwa kunaifanya Serikali kushindwa kutekeleza majukumu yake ipasavyo, kushindwa kuwahudumia wananchi, miradi ya maendeleo  kushindwa kufanyika au kufanyika kwa kiwango

TANZANIA YASHIRIKI MKUTANO WA UPATIKANAJI HAKI NCHINI INDIA

Image
 Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Pindi Chana  akiwa na wajumbe kutoka Tanzania   kwenye  Mkutano wa Upatikanaji Haki uliofanyika tarehe 27- 28  New Delhi,  India . XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Na, George Mwakyembe - WKS Tanzania ni moja kati ya nchi washiriki katika mkutano wa kwanza wa kikanda kuhusu upatikanaji wa msaada wa kisheria, pamoja na Uimarishaji wa upatikanaji Haki katika nchi za ukanda wa kusini. Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana ameongoza washiriki kutoka Tanzania katika mkutano huo uliofanyika New Delhi nchini India kuanzia tarehe 27– 28 Novemba 2023 ukiwa unalenga kujadili masuala ya upatikanaji wa huduma za msaada wa kisheria katika kuimarisha upatikanaji haki nchini. Katika Mkutano huo washiriki walipata nafasi ya kubadilishana uzoefu juu ya utekelezaji wa masuala ya huduma za msaada wa kisheria na jitihada mbalimbali zinazotumika katika kuhakikisha upatikanaji haki katika nchi zao pamoja na kuimarisha uhusiano na   baina   nchi washiriki na

SALVA KIIR MAYARDIT AWASILI NCHINI NA KULAKIWA NA DKT. CHANA

Image
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana na Rais wa Sudan Kusini Mhe. Salva Kiir Mayardit wakikagua gwaride la heshima, tarehe 23 Novemba, 2023 mara baada ya kuwasili nchini. Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana na Mgeni wake Rais wa Sudan Kusini Mhe. Salva Kiir Mayardit mara baada ya kuwasili nchini, tarehe 23 Novemba, 2023 Jijini Arusha. XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir Mayardit amewasili nchini tarehe 23/11/2023 na kupokewa na Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana kushiriki Mkutano wa Kawaida wa 44 wa Jumuiya ya Afrika Mashariki unaofanyika Jijini Arusha. Mara ya mwisho Rais Salva Kiir kuja nchini ilikuwa April 15, 2016 ambapo alikutana na aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia alikuwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Hayati Dkt. John Pombe Magufuli kwa ajili ya utiaji saini wa Mkataba wa Sudani Kusini kujiunga na Jumuiya ya Afrika Mashariki. Mkutano huo unahudhuriwa

WAZIRI CHANA ASHIRIKI KIKAO CHA BARAZA LA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI

Image
  Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akishiriki Mkutano wa Kawaida wa 44 wa Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Afrika Mashariki, tarehe 22 Novemba, 2023 Jijini Arusha. Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akishiriki Mkutano wa Kawaida wa 44 wa Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Afrika Mashariki, tarehe 22 Novemba, 2023 Jijini Arusha. XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana anashiriki Mkutano wa Kawaida wa 44 wa Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Afrika Mashariki unaofanyikia Jijini Arusha. Mkutano huo ulioanzia katika Ngazi ya Wataalam waliokutana Jijini Arusha kuanzia tarehe 18 - 20 Novemba, 2023 na ukafuatiwa na Kikao cha Makatibu Wakuu kilichofanyika tarehe 21 Novemba 2023, kinakamilishwa na Mkutano wa 44 wa Baraza la Mawaziri ulioanza leo tarehe 22 Novemba 2023. Masuala yanayojadiliwa katika Mkutano huo wa wataalam ni pamoja na Taarifa ya Utekelezaji wa maamuzi na maelekezo ya mkutano cha Baraza la Maw

DKT. CHANA AFANYA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA SINGAPORE NCHINI

Image
  Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akifanya mazungumzo na Balozi wa Singapore nchini Mhe. Douglas Foo,  tarehe 20 Novemba, 2023 mtumba, Jijini  Dodoma. Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akikabidhi Balozi wa Singapore nchini Mhe. Douglas Foo mfuko maalum ambao ni rafiki wa mazingira unaotumika kwenye “Mama Samia Legal Aid Campaign” tarehe 20 Novemba, 2023  Dodoma. Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana na Balozi wa Singapore nchini Mhe. Douglas Foo kwenye picha ya pamoja na washiriki kwenye kikao kilichowakutanisha viongozi hao wawili, tarehe 20 Novemba, 2023 Dodoma. XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Na William Mabusi – WKS Dodoma Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana amekutana na Balozi wa nchi ya Singapore nchini Mhe. Balozi Douglas Foo na kufanya mazungumzo kuhusu kuimarisha ushirikiano kwenye sekta mbalimbali na namna ya kubadilishana uzoefu kwenye masuala ya teknolojia. Kikao hicho kimefanyika t

KASI YA UJENZI IENDANE NA UBORA: DKT. CHANA

Image
Mhandisi Nassiri Nassoro akitoa maelezo ya maendeleo ya ujenzi wa jengo la Wizara kwa Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Pindi Chana, tarehe 17 Novemba, 2023 Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akikagua maendeleo ya ujenzi wa jengo la ofisi za Wizara, tarehe 17 Novemba, 2023   XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Na William Mabusi – WKS Dodoma Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana amekagua maendeleo ya ujenzi wa jengo la ofisi za Wizara ambao umefikia asilimia 79 linaojengwa Mji wa Serikali Mtumba Dodoma, na kumtaka Mkandarasi kuongeza kasi huku akizingatia ubora. Ukaguzi huo ameufanya tarehe 17 Novemba, 2023. “Kwenye ujenzi wa majengo haya tunashindana hivyo ukiona mwenzio ameweka vioo nawe unajiuliza la kwangu linawekwa vioo lini,” alisema Dkt. Chana huku akitahadharisha pamoja na mambo mengine upatikanaji wa maji kwenye jengo akitaka kuwepo na uwiano wa idadi ya watumishi na uwezo wa pampu ya kusukumuia maji ili yafike kwenye sakafu zote za jin

MHE CHANA AFANYA KIKAO NA MENEJIMENTI YA WIZARA

Image
  Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Pindi Chana akiongea na menejimenti kwenye kikao kilichofanyika Mtumba, leo tarehe 16 Novemba 2023 jijini Dodoma.  Menejimenti ya Wizara ya Katiba na Sheria wakiwa kwenye kikao cha utekelezaji wa majukumu ya Wizara leo tarehe 16 Novemba 2023. Mtumba jijini Dodoma.  XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Na, George Mwakyembe - WKS – Dodoma Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana amekutana na kufanya kikao na Menejimenti ya Wizara pamoja na watalaam wa sheria kujadili mambo mbalimbali yakiwemo utekelezaji wa   mapendekezo ya haki jinai kwa   Wizara ya katiba na Sheria   pamoja na wasilisho la kutungwa kwa sheria ya kupinga ukatili   wa kijinsia yam waka   2023.   Kikao hicho ambacho kimefanyika leo tarehe 16 Novemba, 2023 katika ofisi za Wizara Mtumba jijini Dodoma, Mhe. Chana amesisitiza watumishi kuhakikisha utekelezajiwa majukumu yaliyoamuliwa yanafanyika kwa ubunifu huku wakizingatia muda.  

MHE. CHANA ATEMBELEA KITUO JUMUISHI CHA MASUALA YA FAMILIA.

Image
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana kwenye picha ya pamoja na badhi ya watumishi wa Kituo Jumuishi cha Masuala ya Familia Temeke, tarehe 15 Novemba 2023.   Naibu Msajili Mfawidhi Kituo Jumuishi Masuala ya Familia Temeke, Mhe. Frank Moshi akimpa maelezo Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Pindi Chana alipotembelea Kituo Jumuishi cha Masuala ya Familia Temeke, 15 Novemba, 2023 Jijini Dar es Salaam. xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana, tarehe 15 November 2023 ametembelea Kituo Jumuishi cha Masuala ya Familia Temeke kukagua shughuli mbalimbali za kiutendaji. Akiwa Kituoni hapo Waziri Chana amepata fursa ya kutembelea maeneo mbalimbali ikiwemo Chumba maalumu ambacho kimetengwa kwa ajili ya akina mama kunyonyesha watoto wachanga wanapofika katika Kituo hicho kupata huduma.

CHANA ASHIRIKI MAADHIMISHO YA MASHUJAA WA VITA YA KWANZA YA DUNIA

Image
  Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt Pindi  Chana , Balozi Wa Uingerza nchini  David Concar  na Balozi wa Ujerumani  Nchini  Wakitoa  heshima  zao kwenye moja ya kaburi la mashujaa waliotoa uhai wao kwenye vita ya kwanza  ya  Dunia. Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt Pindi  Chana , Balozi Wa Uingerza nchini  David Concar  na Balozi wa Ujerumani  Nchini  Wakitoa  heshima  zao kwenye moja ya kaburi la mashujaa waliotoa uhai wao kwenye vita ya kwanza  ya  Dunia XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Na Lusajo Mwakabuku - WKS DSM Waziri wa Katiba n Sheria Mhe.Balozi Dkt Pindi Chana Leo 12/11/2023 ameshiriki Ibada ya maadhimisho ya siku ya Mashujaa waliopoteza maisha wakati wa vita ya kwanza ya Dunia iliyofanyika kwenye makaburi ya Jumuiya ya Madola Kijitonyama Jijini Dar es salaam. Akizungumza katika maadhimisho hayo yaliyoandaliwa kwa ushirikiano baina ya Ubalozi wa Uingereza na Ubalozi wa Ujerumani Waziri Chana amesisitiza kuwa Tanzania itaendelea   kuhamasisha Jamii na

WAZIRI CHANA AIPONGEZA NMB KWA KUTOA HUDUMA ZINAZOIGUSA JAMII

Image
  Waziri wa Katiba na  Sheria  Mhe Balozi Dkt Pindi Chana akiwa katika picha ya pamoja na  Wanasheria Binafsi katika mkutano uliofanyika leo tarehe 10 Novemba Jijini Dar es Salaam . Waziri wa Katiba na  Sheria  Mhe Balozi Dkt Pindi Chanaajiongea na   Wanasheria Binafsi kwenye  mkutano uliofanyika leo tarehe 10 Novemba Jijini Dar es Salaam . Waziri wa Katiba na Sheria  Mhe. Balozi   Dkt Pindi Chana  akipokelewa na mwenyeji wake Afisa Mtendaji Mkuu wa NMB kwenye mkutano wa NMB na Taasisi za Sheria Mkoa wa Dar es salaam.  Waziri wa Katiba naSheria  akiongoza na Mhe Omary Said Shabani  Waziri wa Viwanda na Biashara Zanzibar  baada ya Kuwali kwenye Mkutano wa NMB  na Taasisi  za Sheria  Mkoa wa Dar es Salaam.  Na Lusajo Mwakabuku – WKS Waziri wa Katiba n Sheria Mhe.Balozi Dkt Pindi Chana Ameshiriki Mkutano wa NMB na Taasisi za Sheria za Mkoa wa Dar es Salaam na Kuipongeza Benki hiyo kwa kuendelea kufanya kazi kwa Weledi na kuiomba kuendelea kushiriki kwenye Huduma mbali mbali zinazogusa j

MHE CHANA ASHIRIKI MKUTANO WA TANZANIA - RUSSIA ALUMNI

Image
  Waziri wa Katiba na Sheria  Mhe. Balozi Dkt Pindi Chana akiongea  kwenye mkutano wa Tanzania - Russia  Alumni ulifanyika  leo tarehe 08 Novemba 2023 jijini Dar es salaam.  Waziri wa katika na Sheria  Mhe. Balozi Dkt Pindi Chana  akiongea na Afisa kutoka ubalozi wa Urusi nchini kweny mkutano  wa Tanzania - Russia Alumni ulifanyika leo tarehe 08 novemba  2023 jijini  Dar es salaam. Baadhi wa  watanzania waliosoma nchini Urusi wakiwa kwenye kikao cha Tanzania -Russia Alumni kilichofanyika  Dar es  salaam leo  tarehe 08 Novemba 2023.                           XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Waziri wa Katiba na Sheria Mhe, Balozi Dkt.  Pindi Chana ameshiriki Mkutano wa Wanafunzi waliohitimu Vyuo vikuu vya Nchini Urusi uliofanyika Leo November 08, 2023 jijini Dar es salaam. Akizungumza katika mkutano huo, Mhe. Chana ameipongeza Urusi kwa kuendeleza ushirikiano mzuri na Vyuo vya Tanzania katika Kuboresha Elimu na kuwakaribisha zaidi kuwekeza Tanzania kwani ni sehemu salama. Aidha,k