DKT. NDUMBARO AZINDUA KITABU CHA MIAKA 60 YA UHURU NA SEKTA YA SHERIA


 

XXXXXXXXXXXXXX

Waziri wa Katiba na Sheria Mhe.Dkt.Damas Ndumbaro amepongezwa kwa kusimamia ukamilishwaji wa uandishi na uchapishaji wa Kitabu cha miaka 60 ya Uhuru na Sekta ya Sheria tulipotoka,tulipo na tunapokwenda tangu mwaka (1961 - 2021).

Kitabu hicho kimeweka historia na kumbukumbu  ya miaka 60 kinatoa kipimo tosha  cha maendeleo  katika taasisi mbalimbali za serikali kwa miongo yote 6 tangu uhuru ikiwa ni umri wa mtumishi wa Serikali kustaafu.

Akitoa pongezi hizo wakati wa zoezi la Uzinduzi wa kitabu hicho leo Februari 7,2023 jijini Dodoma,aliyewahi kuwa Waziri wa Katiba na Sheria katika Serikali ya awamu ya tano na  sasa Mbunge wa Jimbo la Kilosa Prof. Palamagamba Kabudi  amesema kuwa historia sio habari ya mambo yaliyopitwa bali ni mambo yaliyopita ambayo yanamwangwi kwa mambo yaliyopo kwa sasa.

"Historia ni habari iliyopita ambayo yanaakisi mambo ya sasa ni chemichemi ambayo jamii iliyaishi,inayaishi na kurithisha kwa vizazi na vizazi kwa kuwekwa katika vitabu,"amesema Pro.Kabudi

Prof.Kabudi amesema kwa miaka mingi historia ya Tanzania imekuwa ya simulizi badala ya kuandikwa ,hivyo kupitia kitabu hicho kitasaidia watu wengi kusoma na kuelewa kiundani kuhusu nchi ilipotoka,ilipo na kupata tathmini inapoelekea  na kufanya vijana wengi wa sasa na baadae kujua jinsi nchi ilivyopiga hatua za maendeleo.

"Kitabu hiki kitasaidia kuzikabili changamoto zilizopo kwa sasa kwa kuyarejea mambo ya zamani ili kupata njia ya kwenda mbele kufikia mafanikio kijamii na kitaifa kwa ujumla.

Kwa upande wake Prof,Sifuni Mchome amesema kuwa kitabu hicho kitasaidia kupima  nchi yote ilipotoka na inapokwenda na ili kufaanikisha hilo kila baada ya miaka mitano kitabu hicho kinakuwa kinachapishwa ili kuongeza historia zinazoendelea kutokea ndani ya miaka hiyo.

"Kitabu hiki kitakuwa kinatoka kwa Edition hii ya kwanza ya miaka 60 na kila baada ya miaka mitano itatoka Edition ya pili nia na mazumuni ni kuendelea kukumbusha historia ya nchi yetu kwa vizazi na vizazi,"amesema  Prof.Mchome

 

Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YAIPONGEZA WIZARA KWA UTEKELEZAJI WA MAMA SAMIA LEGAL AID CAMPAIGN

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA