Mhe. Pauline Gekul amewataka waajiriwa wapya kuwa na uweledi
Naibu
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Pauline Gekul amewataka waajiriwa wapya kuwa na
uweledi, kuepuka vitendo vya ukiukaji wa maadili ya kazi pamoja na kuepuka
rushwa, uonevu na matumizi mabaya ya ajira zao. Mhe. Gekul aliyasema hayo
alipokuwa mgeni rasmi katika hafla ya kufunga mafunzo elekezi kwa waajiriwa
wapya wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka, yaliyofanyika Mkoani Morogoro, Hoteli ya
Kingsway kuanzia tarehe 17-23 Machi, 2023.
Comments
Post a Comment