NAIBU WAZIRI AFANYA ZIARA RITA
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
Na Lusajo Mwakabuku & Josephat Kimaro
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe
Pauline Philipo Gekul (Mb) leo Machi 17, 2023 amefanya ziara na kuzungumza na
Menejimenti ya Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini (RITA).
Kupitia ziara hiyo, Mhe. Gekul amepokea
taarifa ya utekelezaji pamoja na kujengewa ufahamu kuhusu kazi na majukumu ya
Wakala ya kuwahudumia Wananchi kutoka kwa Kabidhi Wasii Mkuu na Afisa Mtendaji
Mkuu wa Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini (RITA) Bi. Angela Anatory.
Mara baada ya kupokea taarifa hiyo, Mhe.
Naibu Waziri ameipongeza RITA kwa mageuzi makubwa wanayofanya kwa kuwezesha
wananchi kuweza kutuma maombi ya huduma kidijitali popote walipo bila kufika
katika ofisi za Wakala. Pia akaitaka RITA kuhakikishwa kwamba a mifumo ya
utoaji huduma inayotengenezwa inakuwa rafiki ili kuwawezesha wananchi hata
wasio kuwa na upeo mkubwa wa teknolojia kuweza kuitumia kwa urahisi kwani wapo
wananchi ambao uelewa wao ni mdogo katika masuala ya matumizi ya mitandao.
Aidha, ameitaka RITA kushirikiana na
wadau wengine kuimarisha usimamizi wa masuala ya Mirathi ili kupunguza migogoro
inayozidi kuongezeka katika jamii huku wananchi wengi wakidhulumiwa haki zao.
Mhe. Gekul pia akaagiza elimu kuhusu mirathi iongezwe ili wananchi waweze kuzitambua
haki zao.
Kwa Mhe. Gekul, hii ni ziara yake ya
kwanza kutembelea taasisi zilizo chini ya Wizara ya Katiba na Sheria tangu
kuteuliwa kwake na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.
Samia Suluhu Hassan kuwa Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mwezi Februari mwaka
huu.
Comments
Post a Comment