Wizara 23 zaungana kutokomeza TB
xxxxxxxxxxxxxxxx
Na,
Lusajo Mwakabuku.
Katika kuhakikisha dhamira ya kupambana
na hatimaye kuitokomeza TB na vichochezi vyake inakamilika, ushirikiano wa Sekta
mbalimbali za Serikali zaidi ya zile zinazohusika na afya pamoja na vipaumbele
thabiti vya kisiasa katika ngazi za juu za uongozi vina nafasi kubwa katika
kuumaliza ugonjwa huu nchini.
Ni kwa mtazamo huo wa Serikali
uliopelekea Wizara 23 kuingia makubaliano ya kuunda Mfumo wa Uwajibikaji wa
Sekta mbalimbali (Multisectoral Accountability
Framework - MAF) uliotiwa Saini na wawakilishi wa Wizara hizo jana
21/03/2023 Jijini Dodoma.
Comments
Post a Comment