Dkt. Ndumabro apokea Taarifa ya Mapitio ya Mfumo wa Sheria
Waziri wa Katiba
na Sheria Mhe. Dkt. Dkt.
Damas Ndumbaro amepokea Taarifa za mapitio ya Mfumo wa Sheria zinazosimamia
Uchaguzi na Vyama vya Siasa Nchini na Mapitio ya Mfumo wa Sheria zinazosimamia
utoaji haki katika Mahakama za Mwanzo kutoka kwa Mhe. January H. Msoffe (Jaji
Mstaafu) Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania. Hafla hiyo imefanyika tarehe 11 Aprili,
2023 Ofisi za Wizara Mji wa Serikali Mtumba Jijini Dodoma. Taarifa hizo
zitawasilishwa Bungeni kwa mujibu wa sheria ili mchakato wa mabadiliko ya
sheria hizo uanze.
Katika hafla hiyo Dkt. Ndumbaro ametoa rai kwa Wizara na Taasisi zote za umma zinazotaka kufanya tafiti, marejeo au uboreshaji wa sheria zao kutumia Tume ya Kurekebisha Sheria kwani ndiyo yenye mamlaka kufanya kazi hiyo
Comments
Post a Comment