DKT NDUMBARO AKEMEA UKATILI WA KINJISIA KONDOA
Mkazi
wa Wilaya ya Kondoa akimweleza jambo Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Damas
Ndumbaro(hayupo pichani) Baada ya Waziri Ndumbaro kufanya ziara ya kukagua
maenedeleo ya Mama Samia legal aid Campain katika Wilaya ya Kondoa tarehe 6 mei 2023
jijini Dodoma.
Wananchi
wa Wilaya ya Kondoa wakiwa wamejitokeza kwenye viwanja vya soko kuu kumsikiliza
Waziri wa Katiba na Sheria Dkt Damas Ndumbaro alipokuwa alipokuwa akitoa
ufafanuzi kuhusu Mama Samia Legal Aid
Campain tarehe 6 mei 2023 jijini Dodoma.
Waziri wa Katiba na
Sheria Dkt Damas Ndumbaro amekemea vikali vitendo vya ukatili wa kijinsia unaojitokeza
katika jamii zetu kwani licha ya kukiuka misingi ya haki za binadamu, vitendo
hivi vinakwenda kinyuma na maadili ya katika jamii zetu zinazotutambulisha kama
watanzania. Dkt ndumbaro ameyasema hayo alipokuwa akito
elimu ya sheria pamoja na msaada wa kisheria kwa wananchi wa Wilaya ya Kondoa
na Chemba Mkoani Dodoma Tarehe 5 Mei, 2023.
Dkt ndumbaro ameyasema
hayo akiwa katika ziara ya ukaguzi wa utekelezaji wa Mama Samia Legal Aid
Campaign kampeni inayolenga kutoa msaada wa elimu ya kisheria unaofanyika
katika wilaya zote mkoani Dodoma tokea Aprili 28 mwaka huu katika wilayo zote
za Dodoma.
Aidha,
Waziri Ndumbaro amesema kuanzia sasa kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi itakuwa
ni siku ya kutoa elimu ya sheria na msaada wa kisheria kwa wananchi.
“Kwa hatua hii ya mwanzo tunaishia tarehe 7
may lakini kwa maelekezo ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kuanzia sasa
kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi uongozi wa wilaya utashirikiana na wizara
kutoa elimu elimu ya sheria na msaada wa sheria kwa wahitaji hususani wananchi
wanyonge ambao wengi wako vijijini.” Alisema Mhe. Ndumbaro.
Mhe. Ndumbaro aliongeza
kuwa Wilaya kwa kushirikiana na timu ya Wizara ya Katiba ya Sheria itakiwa
ikitoa elimu na msaada wa sheria kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi katika kata
itakayopangwa. “Tukimaliza tutaendelea kurudi na kurudi ili kila mtanzania
popote alipo katika kona ya nchi hii lazima apate elimu ya sheria na apate
msaada wa kisheria. Lengo letu ni kuwa baada ya miaka mitatu, kila kata na kila
kijiji kiwe kimefikiwa na huduma hii na wananchi wote wafikiwe na huduma hii
ambayo Rais Samia ameamua kuitoka kwa wananchi bila malipo.”
Vilevile
Dk Ndumbaro alipongeza juhudi za serikali ya awamu ya sita akisema ndani ya
miaka mwili ya uongozi wa Rais Samia kuna mambo makubwa yamefanyika katika
sekta ya sheria ikiwemo kutekeleza kikamilifu Sheria ya Msaada wa Kisheria
iliyotungwa na Bunge mwaka 2017.
“Watanzania
tuna deni la kumuombea kwa Mwenyezi Mungu ammpe afya, uzima aendelee
kututumikia na kujali, tuna deni la kupambana na wale wanaompinga mheshimiwa
Rais na tuna ndeni la kuhakikisha tunaendelea na Rais huyu ifikapo mwaka 2025.”
Kampenzi hii katika
mkoa wa Dodoma ilizinduliwa na Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania
Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb) Aprili 27 jijini Dodoma ambapo ndani ya siku
sita tangu kuanza Kampeni hiyo, wananchi wa kata 10 za Wilaya ya Chemba
wamefikiwa na huduma hii ambapo kwa Wilaya ya Kondoa wananchi zaidi ya 5,000
wamepata elimu na wengine kupewa msaada wa kisheria.
Comments
Post a Comment