TAWLA yafanya Mkutano Mkuu wa 33
Naibu
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Pauline Gekul akihutubia katika Mkutano Mkuu wa
33 wa TAWLA, tarehe 06 Mei, 2023
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
Mhe. Pauline Gekul Naibu Waziri wa Katiba na Sheria ameshiriki
ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa 33 wa Chama cha Wanasheria Wanawake Tanzania (Tanzania
Women Lawyers – TAWLA) uliofanyika tarehe 06 Mei, 2023 Jijini Dar es Salaam.
Mgeni Rasmi katika mkutano huo alikuwa Mhe. Dkt. Tulia Ackson, Spika wa Bunge
la Tanzania.
Katika hotuba yake Naibu Waziri, alisisitiza kuwa Serikali kupitia Wizara ya Katiba na Sheria itaendelea kushirikiana na TAWLA hususan katika kupokea mapendekezo na maoni ya marekebisho mbalimbali ya sheria.
Comments
Post a Comment