MKUTANO WA 77 WA HAKI ZA BINADAMU NA WATU KUFANYIKA JIJINI ARUSHA
XXXXXXXXXXXXXXXXXXX
William
Mabusi - WKS
Naibu Waziri
wa Katiba na Sheria Mhe. Pauline Gekul (Mb) ameongoza timu ya Wizara kwenye
Kikao Kazi kwa ajili ya maandalizi ya Mkutano wa 77 wa Haki za Binadamu na Watu
utakaofanyika hapa nchini mnamo tarehe 20 Oktoba mpaka 9 Novemba,
2023 mkoani Arusha na kuagiza usimamizi mzuri wa maandalizi na uendeshaji
wa mkutano huo.
Kikao Kazi
hicho kimefanyika Jijini Arusha tarehe 28 Juni, 2023 na kuhudhuriwa na Katibu
Mkuu wa Wizara hiyo Bi. Mary Makondo, Mwenyeji Mkuu wa Mkoa wa Arusha Bw. John
Mongella, ndugu Steven Zelothe Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Arusha miongoni
mwa wengine.
Akiongea
katika Kikao Kazi hicho Bi. Makondo alielezea chimbuko la Mkutano huo na
alisema ni heshima kwa nchi kuwa mwenyeji wa Mkutano huo akibainisha kuwa nchi
itanufaika kijamii, kiuchumi, kidiplomasia na haki za binadamu.
Akitoa
shukrani zake kwa Wizara, Mkuu wa Mkoa ameishukuru Wizara ya Katiba na Sheria kwa
kuchagua Mkoa wa Arusha kuwa mwenyeji wa mkutano huo mkubwa unaoangazia masuala
ya haki za binadamu na watu.
Comments
Post a Comment