Tufanye kazi na kushiriki kwenye Michezo: Dkt. Ndumbaro


Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akipokea medal ambazo Wizara ilishinda kwenye Marathon ya miaka 60 ya JKT, tarehe 27 Juni, 2023.

Watumishi wa Wizara ya Katiba na Sheria wakiwa kwenye hafla ya kuwapongeza watumishi walioshiriki kwenye marathon ya miaka 60 ya JKT, tarehe 27 Juni, 2023.

                                           XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX

Na William Mabusi - WKS

Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) amesisitiza watumishi wa Wizara hiyo pamoja na kutekeleza majukumu yao lakini pia washiriki kwenye michezo kwani michezo huimarisha afya.

Dkt. Ndumbaro ameyasema hayo tarehe 27 Juni, 2023 wakati wa hafla ya kuwapongeza watumishi walioshiriki kwenye marathon ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kufikisha miaka 60 iliyofanyika tarehe 25 Juni, 2023 ambapo Wizara ilishiriki na kuwa miongoni mwa Wizara zilizopata Medali, Mgeni Rasmi kwenye marathon hiyo alikuwa Rais wa Awamu ya Nne Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete.

Aidha, Waziri alisisitiza watumishi kufanya kazi kwa kushirikiana na kutekeleza majukumu kwa wakati, “tumia kipaji chako katika kutimiza majukumu yako kwa dhati kabisa. Hatuna sababu za kuchelewesha kazi, unalipwa kwa sababu unafanya kazi na si ulipwe kwa sababu umeajiriwa.” Alisema Dkt. Ndumbaro huku akiwataka watumishi hao kujiandaa na jukumu kubwa lililo mbele yao la Katiba Mpya.

Akiongelea kuhusu ushiriki wa michezo, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Bi. Mary Makondo alisema Wizara itaendelea kushiriki katika michezo mbalimbali na ana matarajio makubwa kuhusu ushiriki na kufanya vizuri kwa Wizara ya Katiba na Sheria kwenye michezo ijayo ya SHIMIWI.

 


Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YAIPONGEZA WIZARA KWA UTEKELEZAJI WA MAMA SAMIA LEGAL AID CAMPAIGN

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA