Wizara imejipanga kuendelea kujenga Mahakama nchini - Pauline Gekul.
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mh.Pauline Gekul aitoa ufafanuzi wa swali aliloulizwa na mbunge wa kigoma kusini mheshimiwa Nashon Bindyanguze leo tarehe 20 juni 2023 Bungeni Dododma.
XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX
Na. George Mwakyembe. WKS – Dodoma.
Naibu Waziri wa
Katiba na Sheria Mhe. Pauline Gekul amesema Wizara imejipanga kundelea na
ujenzi wa Mahakama nchini kwa mwaka wa bajeti 2023/2024 na tayari Wizara imejipanga
kujenga zaidi ya mahakama 60.
Mheshimiwa Gekul amesayema
hayo alipokuwa akijibu swali la mbunge wa Kigoma mheshimiwa Nashoni Bindyanguze
mbunge wa Kigoma Kusini. Mheshimiwa Gekul amesema kwa mwaka wa bajeti 2024/2025
Wizara itajenga Mahakama ya Mwanzo katika eneo la Mgambo ambalo ndiyo makao
makuu ya Tarafa ya Buhingu.
Naye mbunge wa
Arusha mjini Mhe. Mrisho Gambo aliuliza swali la nyongeza kwa mheshimiwa Naibu
Waziri Gekul kutaka Kujua ujenzi wa mahakama ya mwanzo katika kata ya Terati.
Mheshimiwa Gekul amemhakikishia kuwa katika mwaka wa fedha 2023/2024 ujenzi wa
mahakama tayari kata ya Terati ni kata mojawapo ambayo ujenzi huo utajengwa.
Mbunge wa Viti
maalumu Mkoa wa Manyara Mhe. Asia Halamga aliuliza swali kutaka kujua ujenzi wa
mahakama eneo la mijingu Mkoani Manyara. Mhe. Naibu Waziri Gekul amemtoa
wasiwasi na kwamba hilo eneo tayari liko kwenye mpango wa ujenzi wa mahakama
kwa mwaka fedha unaokuja.
Naye mbunge wa
viti maalumu Mkoa wa Shinyanga
Mheshimiwa Christine Mzava ameomba Wizara kufanya ukarabati wa mahakama za kata ya Usanda na Samuye kwani
zimejengwa tokea enzi za mkoloni, Mheshimiwa Gekul amemhakikishia kuwa mahakama hizo zitafanyiwa ukarabati .
Comments
Post a Comment