Wizara ya Katiba na Sheria yakutana na Sekretarieti ya Jumuiya ya Madola
Wawakilishi kutoka RITA wakifafanua jambo kuhusu namna taasisi ya RITA inavyofanya kazi wakati wa kikao na Sekretarieti ya Jumuiya ya Madola. Tarehe 28 Juni 2023 Jijini Dodoma
George
Mwakyembe- WKS
Wizara ya Katiba na Sheria wamefanya kikao na Sekretarieti ya Jumuiya ya Madola. Katika kikao hicho ambacho kimeongozwa na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Huduma za Sheria kwa Umma Ndg. Abdulrahman Mshamu akimwakilisha Katibu Mkuu wa Wizra ya Katiba na Sheria.
Katika kikao
hicho ambacho kimefanyika leo tarehe 28 Juni 2023 Jijini Dodoma. Sekretarieti
hiyo imeipongeza Tanzania kwa kuendelea kuwa daraja la kwanza katika kutekeleza
Haki za Binadamu. Hizi juhudi kubwa zinazofanywa na Serikali ya awamu ya sita
inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuhakikisha Haki za Binadamu zinatekelezwa
pamoja na kulindwa.
Akiongea
kwenye kikao hicho Mwenyekiti wa Sekretarieti Bi. Evelyn Pedersen amesema “kwa thatmini
ambayo tumekuwa tukifanya kwa nchi za Jumuiya ya Madaola tunategemea kujengeana
uwezo baina ya Tanzania na nchi wanajumuiya ya Madola katika masuala mbalimbali
yahusuyo jamii zetu ni vyema tukaangalia wapi tunatakiwa kupafanyia kazi ili
tuweze kushirikiana.”
Mwenyekiti
huyo amesema “Katika nchi wanajumuiya ya Madola, Tanzania ni nchi ya kuigwa
hasa katika kuimarisha amani, umoja na utulivu wa wananchi wake na hii
inatupelekea kupanga kufanya kikao cha Mawaziri wa nchi za Jumuiya za Madola
hapa nchini ifikapo mwakani ambacho kitajadili masuala mbalimbali yahusuyo nchi
zetu”
Comments
Post a Comment