Bi. Makondo afanya mazungumzo na Ujumbe wa Ubalozi wa Marekani


 

 Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Bi. Mary Makondo  akiongea jambo alipokutana na kufanya mazungumzo na Ujumbe kutoka Ubalozi wa Marekani nchini, tarehe 17 Julai, 2023 Mtumba Jijini Dodoma.


Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Kisheria kwa Umma Bw. Abdulrahman M. Mshamu akitoa salaam za ukaribisho kwenye kikao ambacho Katibu Mkuu wa Wizara Bi. Mary Makondo alifanya mazungumzo na Ujumbe kutoka Ubalozi wa Marekani, 17 Julai, 2023 Ofisi za Wizara Mtumba, Dodoma

Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Bi. Mary Makondo (kulia), akipokea mfuko wa kitambaa ambao ni rafiki kwa mazingira kutoka kwa Wageni wake waliotoka Ubalozi wa Marekani Balozi Michele Sison (kushoto) na Prof. Sarah Cleveland (katikati), 17 Julai, 2023. Ofisi za Wizara Mtumba Jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Bi. Mary Makondo (kulia), kwenye picha ya pamoja na Wageni wake kutoka Ubalozi wa Marekani Balozi Michele Sison (kushoto) na Prof. Sarah Cleveland (katikati), 17 Julai, 2023. Ofisi za Wizara Mtumba Jijini Dodoma.

                                           xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

Na, William Mabusi-WKS 

Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Bi. Mary Makondo akiwa na Menejimenti ya Wizara hiyo amekutana na kufanya mazungumzo na Ujumbe kutoka Ubalozi wa Marekani nchini ulioongozwa na Balozi Michele Sison kwenye Ofisi za Wizara Mtumba Jijini Dodoma tarehe 17 Julai, 2023.

Katika mazungumzo yao pande zote mbili zimepongeza ushirikiano uliopo kati ya Tanzania na Marekani kwenye nyanja mbalimbali na kutaka ushirikiano huo uendelee pia kwenye sekta ya sheria kwa kuwajengea uwezo wa wataalamu wa ndani katika masuala ya utatuzi wa migogoro kwa njia mbadala, uandishi wa mikataba na kufanya tafiti kwenye uandishi wa mikataba ya kimataifa.

Aidha, Ujumbe huo umepongeza jitihada zinazofanywa na Serikali ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye maboresho ya sheria mbalimbali nchini kwa manufaa ya watanzania.






Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YAIPONGEZA WIZARA KWA UTEKELEZAJI WA MAMA SAMIA LEGAL AID CAMPAIGN

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA