MAAMUZI YA MAHAKAMA HAYAANGALII UNYONGE WA MTU
Mhe. Jane Pascal Mudogo Hakimu Mkazi Mahakama ya Mwanzo Nakapanya akitoa mada ya sheria kwenye utekelezaji wa Mama Samia Legal Aid Campaign Kata ya Nanjoka tarehe 24 Julai, 2023 Tunduru
Bi. Blandina Adam Sekela Afisa Ustawi wa Jamii Wilaya ya Tunduru akitoa mada ya ukatili wa kijinsia kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari Frank wilayani Tunduru, 24 Julai, 2023
Bi. Blandina Adam Sekela Afisa Ustawi
wa Jamii Wilaya ya Tunduru akiimba wimbo wa “usiniguse hapa” na wanafunzi wa
shule ya Msingi Nanjoka wilayani Tunduru, 24 Julai, 2023.
Mwanafunzi Salma Mbunya wa darasa la tano akiishukuru timu ya Mama Samia
Legal Aid Campaign iliyofika shuleni hapo kutoa elimu ya ukatili wa kijinsia na
haki na wajibu wa mtoto, 24 Julai, 2023 Tunduru.
XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX
Na William Mabusi – WKS Tunduru
Timu inayotekeleza Mama Samia Legal Aid Campaign Wilayani
Tunduru katika Mkoa wa Ruvuma imesema maamuzi ya Mahakama hayatolewi kwa
kuangalia fulani ana uwezo na kumpa haki hata kama yeye ndiye mwenye makosa
bali haki hutolewa kwa mujibu wa sheria na kadri ushahidi ulivyotolewa.
Hayo yamesemwa na Wakili Jane Lyimo kutoka
Wizara ya Katiba na Sheria wakati akitoa mada ya sheria kwenye mkutano wa
hadhara uliofanyika viwanja vya ofisi za Kata ya Nanjoka Wilayani Tunduru
tarehe 24 Julai, 2023.
“Maamuzi ya Mahakama hayaangalii mtu
mwenye uwezo apewe haki na yule asiye kuwa na uwezo kunyang'anywa haki yake.
Hali ya unyonge wa mtu haisababishi yeye kukosa haki yake kisheria.” Alisema
Bi. Lyimo.
Aidha, Bi. Lyimo aliwashauri wananchi kama
wana uthibitisho wa matukio yenye viashiria vya rushwa kutoa taarifa hizo
kwenye vyombo vingine vya haki kama TAKUKURU na Polisi.
Akichangia mada hiyo Mhe. Jane Pascal Mudogo
Hakimu Mkazi Mahakama ya Mwanzo Nakapanya amesema sheria inaruhusa mtuhumiwa
kubadilishiwa Hakimu endapo hana imani naye lakini pia Mahakama imeanzisha
Madawati ya kupokea malalamiko ili wananchi wanaokutana matukio yenye viashiria
vya rushwa kutoa taarifa hizo huko.
Mkutano huo uliwahusisha wananchi kutoka
Vijiji vya Nanjoka, Uwanja wa ndege na NHC, ulifanyika ofisi za Kata ya
Nanjoka, Halmashauri ya Tunduru ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Kampeni ya
Kitaifa ya Mama Samia inayolenga kutoa elimu ya sheria na msaada wa sheria kote
nchini.
Baadaye timu hiyo ilitembelea shule ya
Sekondari ya Frank na shule ya Msingi Nanjoka kutoa elimu juu ya haki na wajibu
wa mtoto pamoja na mada kuhusu ukatili wa kijinsia. Akitoa shukrani kwa timu ya
Mama Samia Legal Aid Campaign kutoa elimu hiyo shuleni kwao mwanafunzi Salma
Mbunya wa darasa la tano alisema “nawashukuruni kwa kutupa elimu ya mambo ya
ukatili wa kijinsia ambayo tukikutana nayo tunajua wapi pa kupata msaada nasisi
tutatoa elimu hiyo kuwaelimisha wenzetu.”
Comments
Post a Comment