TUPINGE NDOA ZA UTOTONI NI ADUI WA NDOTO ZA MABINTI WETU.


Mkurugenzi msaidizi wa Haki za Binadamu Ndg. Richard Kilanga akiongea na Wananchi wa kijiji cha Mtipwili kuhusu ukatili wa kijinsia, miradhi, migogoro ya ardhi pamoja na ndoa za utotoni wakati wa utekelezaji wa Mama Samia Leagal Aid Campain Wilaya Nyasa Mkoa wa Ruvuma.

Msaidizi wa kisheria ndugu Nurdin Shabani  akiongea na wanafunzi wa shule ya msingi mitenje iliyopo kata mtipwili kuhusu ukatili wa kinjisia pamoja na haki za watotowakati wa utekelezaji wa kampeni ya mama samia msaada wa kisheria Wilaya ya Nyasa Mkoani Ruvuma.


                                      
Mkurugenzi Msaidizi Wa haki za Binadamu ndugu Richard Kilanga akiongea na Wananchi wa kata ya Mtipwili Wilaya ya Nyasa wakati wa utekelezaji wa Kampeni ya Mama samia msaada wa kisheria.

                                                 XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX

Na, George Mwakyembe – Nyasa

Mkurugenzi Msaidizi wa idara ya Haki za binadamu kutoka Wizara ya Katiba na Sheria Ndg. Richard Kilanga amesema ni lazima jamii zetu ziungane kupinga vikali suala ukatili wa kijinsia.

Hayo amesema jana alipokuwa akiongea na wananchi wa kata ya Mtipwili Wilaya ya Nyasa Mkoani Ruvuma. Ndg Kilanga amesema “ifike wakati sasa jamiii yetu tuungane kupinga na kutokomeza suala la ndoa za utotoni, watoto wetu wanapewa mimba na watu ambao tunawajua lakini baadhi yetu kwenye jamii zetu   hawatoi ushirikiano pale mtoto anapopata mimba kwa kuhofia au kupewa chochote kitu. Hili suala haliwezekani lazima tisimame kwa pamoja na kukemea vitendo hivi kwa nguvu ya pamoja.

Aidha Ndg Kilanga amesema “unapoona mwanafunzi au mtoto kapewa mimba basi toa taarifa mapema kwa vyombo husika ikiwemo polisi ili hatua za kisheria zichukuriwe haraka sana. Ndoto za watoto wetu lazima zitimie bila kukatishwa.

Akiongea na wananchi wa kata ya Mtipwili kijiji cha Malini Bw. Kilanga amesema katika wilaya ya Nyasa ndoa za utotoni ni tatizo kubwa sana lakini wananchi wamekuwa wakilifumbia macho, hili sula halikubaliki kabisa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amekuwa mstari wa mbele kukemea vitendo hivi vya ukatili wa kijinsia ikiwemo ubakaji, ulawiti pamoja na  vitendo vyote ambavyo ni ukatili wa kijinsia ndiyo maana Mheshimiwa Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan  katutuma kukemea pamoja na kutoa elimu dhidi ya ukatili wa kijinsia na ndoa za utotoni   pamoja na kutatua migogoro ya ardhi ambayo pia imekuwa kero kubwa sana katika jamii zetu.

Kampeni ya Mama Samia Legal Aid inaendelea baada ya kuzuduliwa na Makamu wa Rais Dkt Philip Mpango tarehe 22 Julai Mkoani Ruvuma. Kampeni hiyo ambayo inafanyika katika Wilaya zote za Mkoa Ruvuma imekuwa msaada mkubwa sana  kwa jamii zetu katika kutatua matatizo mbalimbali yanayowakabili wananchi. Kampeni ya Mama Samial Legal Aid kwa Mkoa wa Ruvuma itafikia tamati tarehe 2 agosti 2023.

 



Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YAIPONGEZA WIZARA KWA UTEKELEZAJI WA MAMA SAMIA LEGAL AID CAMPAIGN

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA