DKT NDUMBARO AFUNGUA KIKAO CHA MAJADILIANO CHA MCHAKATO WA WA KATIBA MPYA

Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Damasi Ndumbaro  akiongea kwenye kikao cha Majadiliano ya  Katiba mpya  na Mkakati wa Taifa wa Elimu ya Katiba   kilichofanyika kwenye ukumbi Hyatt   Regency  leo tarehe 28 Agosti Jijini Dar es Salaam .

Katibu Mkuu wa Wizara Katiba na Sheria Bi. Mary makondo  akiongea kwenye kikao cha Majadiliano ya  Katiba mpya  na Mkakati wa Taifa wa Elimu ya Katiba   kilichofanyika kwenye ukumbi Hyatt   Regency  leo tarehe 28 Agosti Jijini Dar es Salaam .


Makamu wa kwanza wa Zanzibar wa Rais wa Serkali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Othamn Masoud Othaman akiwa katika picha ya pamoja na  Mawaziri wakuu wataafu ,  pamoja na meza kuu ( waliosimama )  kwenye kikao Majadiliano ya  Katiba mpya  na Mkakati wa Taifa wa Elimu ya Katiba   kilichofanyika kwenye ukumbi Hyatt   Regency  leo tarehe 28 Agosti Jijini Dar es Salaam .

xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

Na George Mwakyembe na Lusajo Mwakabuku - WKS- Dar es Salaam.

Waziri wa Katiba na Sheria Dkt Damasi Ndumbaro ameongoza Kikao cha Mawaziri wa Sheria na Wanasheria Wakuu wa Serikali Wastaafu na waliopo Madarakani kuhusu Majadiliano ya Mchakato wa katiba Mpya pamoja na Mkakati wa Elimu ya Katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977

Akizungumza wakati akifungua kikao hicho tarehe 28 Agosti 2023 Jijini Dar es salaam Dkt Ndumbaro amesema lengo la kikao hicho kilikuwa ni kujadili mchakato wa katiba mpya pendekezwa ulioanza 2014 ambao bado haujafikia muafaka.

Dkt Ndumbaro ameongeza kuwa kikao hicho kimelenga kuongeza uelewa na kutoa elimu juu ya Mwenendo wa Mchakato wa Katiba mpya.

"Wizara kwa kutambua baadhi ya wananchi kudai Katiba mpya, uwepo wa Tume huru ya uchaguzi na Utawala unaozingatia Haki za Msingi za Binadamu na mambo mengine mengi ambayo yanahusisha shughuli za kimaendeleo, siasa na Katiba ya nchi. Kutokana na kuongezeka kwa hoja hizo na viashiria vya jamii kutofahamu haki za kikatiba, baadhi ya watu kujichukulia sheria mikononi, kushindwa kuheshimu utawala wa sheria na kutokujua wajibu wao kwa Taifa, hali inayopelekea kuwepo kwa mahitaji ya kuweka muongozo wa utoaji wa elimu ya Katiba katika masuala ya Haki za Binadamu na Haki na wajibu kwa jamii ya watanzania katika ngazi zote za kiutawala" amesema Waziri Dkt.  Ndumbaro. 

Dkt Ndumbaro alifafanua baadhi ya majukumu ya Wizara kwenye kikao hicho kuwa   ni Kuratibu mchakato wa Katiba ya Mwaka 1977 kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ikiwemo mawaziri wastaafu wanasheria na wale waliopo madarakani kupata mrengo mmoja uliokusudiwa 

"Nimefungua kikao hiki Leo ili kupitia kikao hiki tupate maoni yenu kwa upande wa Zanzibar na Tanzania bara kufahamu wapi kulitakiwa kufanyiwa marekebisho katiba ya 1977 " Ameongeza Dkt. Ndumbaro.

 


Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YAIPONGEZA WIZARA KWA UTEKELEZAJI WA MAMA SAMIA LEGAL AID CAMPAIGN

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA