HUDUMA YA MSAADA WA KISHERIA KUWA ENDELEVU.
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt Damas Ndumbaro akitoa ufafanuzi wa jambo alipokuwa akiongea na Mkurugenzi Mtendaji wa LSF Bi Lulu Ng'wanakila tarehe 03 Agost 2023 Jijini Dar es salaam.
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
Na Felix Chakila - WKS Dar es Salaam
Waziri wa
Wizara ya Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro amekutana na kufanya
mazungumzo na Uongozi wa Mtandao wa Watoa Huduma ya Msaada wa Kisheria (TANLAP)
na Menejimenti ya Legal Services Facility “LSF” tarehe 03 Agosti, 2023 jijini
Dar es Salaam na kujadili masuala ya msaada wa kisheria na ufahamu wa masuala
ya sheria ili kuona namna ya kuwa huduma ya msaada wa kisheri inavyokua
endelevu nchini.
“Ni vyema
mara baada ya kutekeleza Kampeni ya Mama Samia ya Msaada wa Sheria katika mkoa
husika kukawa jitihada za kuifanya Kampeni kuwa endelevu ili wanachi waendelee
kupata huduma. Niwasihi TANLAP na wadau wengine wakiwemo Chama cha Wanasheria
Tanganyika kutumia Ofisi ambazo zipo katika maeneo husika na kuwezesha migogoro
iliyoibuka iweze kushughulikiwa.” Alisema Dkt. Ndumbaro.
Katika mazungumzo hayo, Uongozi wa TANLAP umewasilisha
ombi kwa Serikali kuendelea kuangalia kwa jicho la ukaribu Sheria zinazohusu
ndoa na mirathi kwa kuwa zimekua zikiongezeka kwa kiwango kikubwa na pia ipo
haja ya Serikali kuongeza rasilimali watu katika Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki
cha Temeke kinachoshughulikia migogoro ya Mirathi na Ndoa.
Comments
Post a Comment