KAMATI YAPOKEA TAARIFA YA UTENDAJI WA WIZARA NA TAASISI ZAKE


 Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Pauline Gekul akitoa ufafanuzi kwenye kikao na ya Kamati ya Kudumu ya bunge Katiba na Sheria wakati wa kuwasilisha taarifa ya utekelezaji ya Wizara kwenye ukumbi wa bunge leo tarehe 22 Agosti 2023.Jijini Dodoma

Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakifuatilia uwasilishwaji wa taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya Wizara  kwenye kikao kilichofanyika leo tarehe 22 Agosti 2023. Kwenye ukumbi wa bunge Jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Bi. Mary Makondo akitoa ufafanuzi wa taarifa kwenye kikao cha Kamati ya kudumu ya Utawala, Katiba na Sheria leo tarehe 22 Agosti 2023. Jijini Dodoma.

XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX

Na. George Mwakyembe, Emmanuel Msenga, WKS – Dodoma.

Kamati ya Kudumu ya Utawala na Katiba na Sheria imepokea taarifa ya utendaji wa Wizara na Taasisi zake na kuipongeza Wizara namna inavyosimamia Taasisi zake katika kutekeleza majukumu yake ikisema kuwa taarifa  inaonesha Wizara  imekuwa na Ushirikiano wa karibu  na Taasisi  zake ili kuhakikisha utendaji wa kazi unafanyika  kwa weledi na kushirikiana.

Akiongea kwenye kikao cha kupokea taarifa ya miezi miatatu ya utekelezaji wa majukumu ya Wizara pamoja na Taasisi kwa kipindi cha miezi mitatu zilizo chini ya Wizara leo tarehe 22 Agosti 2023 Jijini Dodoma.  Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya bunge ya Utawala, Katiba na Sheria Mhe. Dkt Joseph Mhagama (MB) amesema naipongeza Wizara kwa jitahada nzuri zinafanywa kwa kusimamia Taasisi na kujenga shirikiano ambao umekuwa na mafanikio katika majukumu yenu”

Katika kikao hicho viongozi wa Taasisi wamefanikiwa kuwasilisha mafanikio yao na changamoto za Taasisi zao, Taasisi zilizowasilisha taarifa ya utendaji ni Tume ya Utumishi wa Mahakama, Ofisi ya Serikali ya Mwendesha Mashtaka, Tume ya Kurekebisha Sheria, pamoja na Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) ambao wote walielezea mafanikioa na changamoto zinazowakabili wakati wa utekelezaji wa majukumu. Moja ya changamoto ambayo imekuwa mtambuka kwa taasisi zote ni upungufu wa rasilimali watu. Akijibu maswali yalioulizwa na wajumbe Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Bi Mary Makondo amesema Wizara pamoja na Taasisi bado idadi ya watumishi haitoshi na majukumu yamekuwa mengi na watumishi wamekuwa wakijotoa kufanya kazi hadi muda wa ziada.

Aidha mjumbe wa Kamati Mhe. Dkt Kaijage amezisisitiza Taasisi hizo kushughulikia masuala mbalimbali ya wafanyakazi wa Wizara na taasisi hizo, ikiwemo upatikanaji wa makazi ya wafanyakazi, kupandishwa vyeo wafanyakazi wao wenye sifa, “Kuna wafanyakazi ambao hawajapandishwa madaraja muda mrefu sana hao muwapandishe ili kuwapa morali na kazi, alisema Mhe. Kaijage.

Naye Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Pauline Gekul, ameishukuru Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kwa pongezi pamoja na maoni ya kuhusu taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya Wizara na Taasisi hizo, na kuahidi kuendelea kushirikiana bega kwa bega na taasisi hizo ili kuimarisha utendaji wa taasisi hizo ambazo zina manufaa kwa wananchi.

“Tukushukuru Ndugu Mwenyekiti pamoja na wajumbe wa kamati hii kwa maoni yenu, sisi kama Wizara pamoja na taasisi zetu zote niwaahidi tutayafanyia kazi maoni haya, na kuongeza ushirikiano baina yetu ili kuboresha utendaji zaidi”

Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YAIPONGEZA WIZARA KWA UTEKELEZAJI WA MAMA SAMIA LEGAL AID CAMPAIGN

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA