MAKONDO AFANYA ZIARA YA KIKAZI IRINGA
Bi Mary Makondo ( katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na watalaamu kutoka PPPRA baada kumaliza mafunzo ya mfumo wa manunuzi NeST yanayoendelea Mkoani Iringa . Kushoto kwakwe ni Naibu katibu Mkuu Dkt Khatibu Kazungu .
XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX
Katibu Mkuu wa Katiba na Sheria Bi Mary Makondo amefanya ziara ya kikazi mkoani Iringa ambapo katika ziara hiyo amefanikiwa kushiriki mafunzo ya mfumo wa NeST yaliyotolewa na wataalam kutoka PPRA.
Aidha, Katibu Mkuu ametembelea timu ya Wataalam wa PPRA wanaojenga na kutoa huduma za mfumo wa NeST na akawapongeza pia akiwataka waongeze juhudi katika kuhakikisha mfumo unakuwa rafiki na hivyo kuboresha taratibu za manunuzi zitakazowezesha taifa kuboresha huduma za serikali kwa wananchi kwa ujumla.
Katika hatua nyingine akiwa Mkoani Iringa, Bi Makondo ametembelea na
Kuzungumza na Wafanyakazi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Mkoani Iringa na
kujadili mambo mbalimbali yahusuyo utendaji wao wa kazi, Muono Mbele, mafanikio
na Changamoto zao.
Comments
Post a Comment