MHE GEKUL AONGOZA KIKAO CHA KUJADILI MPANGO KAZI WA TAIFA WA HAKI ZA BINADAMU NA BIASHARA


      Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Pauline Gekul akihutubia katika kikao cha kujadili  Mpango kazi wa Taifa wa Haki za Binadamu na Biashara, kilicho anadaliwa na Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora kwa Kushirikiana na Shirika na Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), katika ukumbi wa  Morena Hotel  tarehe 25 Agosti 2023 jijini Dodoma.

       Katibu Mtendaji wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Bw. Patience K. Ntwina, akizungumza wakati wa kikao cha Kujadili mpango Kazi wa Taifa wa Haki za Binadamu na Biashara kilichoandaliwa na Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa, leo tarehe 25 Agosti 2023, katika ukumbi wa Hoteli ya Morena jijini Dodoma.

 Wawakilishi wa Wizara na Taasisi mbalimbali, wakifuatilia Kikao cha kujadili  Mpango kazi wa Kitaifa wa Haki za Binadamu na Biashara, ulioandaliwa na Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora kwa Kushirikiana na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), katika ukumbi wa Hoteli ya Morena leo tarehe 25 Agosti 2023 jijini Dodoma.

 Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Pauline Gekul, akiwa katika picha ya pamoja na Menejimenti ya Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Wawakilishi wa Wizara pamoja na  Taasisi mbalimbali mara baada ya Kikao cha Kujadili Mpango Kazi wa Taifa wa Haki za Binadamu na Biashara kilicho andaliwa na Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Agosti 25, 2023 jijini Dodoma.

            XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX

     Na, George Mwakyembe, Emmanuel Msenga, Faraja Mhise - WKS

Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Pauline Gekul (MB) ameongoza kikao cha kujadili mpango kazi  wa Taifa  wa Haki za Binadamu na Biashara (National Action Plan on Business and Human Right in Tanzania Mainland and  Zanzibar) kilicholenga kuangazia masuala ya Haki za Binadamu  hasa kwenye nyanja ya biashara  kama vile uwekezaji  pamoja na shughuli zingine za kibiashara huku ukizingatia masaula ya haki za binadamu wakati wa utekelezaji wake.  

Kikao hicho ambacho kimehusisha  Wizara  na Taasisi mbalimbali  kimefanyika tarehe 25 Agosti 2023 katika ukumbi wa Morena Jijini Dodoma. 

Akizungumza katika kikao hicho, Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Pauline Gekul, ambaye alilkuwa mgeni rasmi ameipongeza Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora kwa kushirikiana vyema na Wizara mbalimbali, Idara za Serikali, Taasisi za Umma, Sekta binafsi, Asasi za kiraia, pamoja na wafanyabiashara na wadau wa maendeleo ya jamii kwa ujumla. 

Mhe. Gekul ameongeza kuwa  malengo ya Kikao hiki ni moja kati ya hatua zinazochukuliwa na Serikali kupitia Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora kushirikisha wadau mbalimbali katika mchakato wa kuandaa mpango wa kitaifa wa Haki za Binadamu na biashara pamoja uwekezaji.

Aidha , Mhe Gekul ameitaja Tanzania, kuwa ni moja kati ya nchi kumi zilizoanzisha mpango huu, kati ya Nchi hamsini na nne za Afrika. 

Wakati huohuo Gekul ameipongeza Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora kwa kupata hadhi ya daraja ‘A’, ya Mtandao wa Taasisi za Kimataifa za Haki za Binadamu ulimwenguni.

Naye Makamu Mwenyekiti  wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Mohamed Khamis Hamad aligusia ukuhimu wa masuala ya haki za binadamu katika uwekezaji ili kuondoa manyanyaso na ukiukwaji haki

“Ni vyema uwekezaji ukazingatia Haki za Binadamu  na kuzilinda , tayari nchi za Kenya  na Uganda walisha andaa mpango  kazi huo na  sasa wapo kwenye utekelezaji”.

Akiongea kwenye kikao hicho, Mshauri wa masuala ya utawala bora kutoka shirika la Maendele la umoja wa matafa Bw. Godfrey Mulisa amesema Haki za Binadamu na biashara  ni uwanja mpana sana  utakaowasaidia wafanyabiashara  katika ufanyaji wa biashara zao huku wakizingatia haki za Binadamu. 

Pia ameahidi kuwa umoja wa mataifa wataendelea kushirikiana na Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora katika utakelezaji wa mpango kazi  huu.

Aidha, Katibu Mtendaji wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Bw. Patience Ntwina ameishukuru Wizara ya Katiba na Sheria pamoja na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa kwa ushirikiano wanaowapa katika kutekeleza suala zima la Haki za Binadamu. Pia Bw. Ntwina ameongeza kuwa mchakato wa kuandaa mpango kazi wa Haki za Binadamu na biashara  umetokana na andiko ambalo liliwasilishwa katika Wizara ya Katiba na Sheria baada ya kufanyika vikao kadhaa ambapo walipendekeza kuwepo na majadiliano ambayo yatawahusisha wadau mbalimbali ili kufanikisha mpango kazi huu hivyo leo ni fursa kutoa mapendezo na maoni ili kuweza kuboresha mpango kazi huu  kwa maendeleo endelevu ya Taifa.

Kikao hicho ambacho kimeandaliwa na Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora(CHRAGG) kwa kushirikiana na Shirika la Maenedeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) kwa lengo la kuwajengea uelewa wa kuzingatia masauala ya Haki za Binadamu wakati wa utekelezaji wa biashara na uwekezaji.

 

 

Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YAIPONGEZA WIZARA KWA UTEKELEZAJI WA MAMA SAMIA LEGAL AID CAMPAIGN

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA