TEHAMA ITAIMARISHA UTAOJI WA MSAADA WA KISHERIA - MAKONDO
Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Bi Mary Makondo akiongea na Watalamu wa TEHAMA katika ukumbi wa Morena leo tarehe 22 Agosti 2023
XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX
Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Bi. Mary Makondo amezindua mafunzo ya Mifumo ya TEHAMA yaliyoandaliwa na Shirika la Mtandao wa watoa huduma za Msaada wa Kisheria la (TANLAP) iliyofanyika leo Agosti 22, 2023 Jijini Dodoma.
Akiongea katika hafla hiyo
iliyofanyika katika Ukumbi wa mikutano wa Hoteli ya Morena, Katibu Mkuu
amesisitiza matumizi ya TEHAMA katika kuwafikia wanyonge na kuwapa huduma za
msaada wa Kisheria kote nchini huku akiwaasa washiriki wa mafunzo haya
kushiriki kikamilifu Kampeni ya Kitaifa ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia
yaani Mama Samia Legal Aid Campaign.
Comments
Post a Comment