Mhe. Balozi
Dkt. Pindi Chana kwenye picha ya pamoja baada ya kufanya mazungumzo na Balozi
wa Urusi nchini Mhe. Andrey Avetisyan. 27/09/2023 Jijini Dar es Salaam.
Balozi wa
Urusi nchini Mhe. Andrey Avetisyan (kulia) alipokutana na kufanya mazungumzo na
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana. 27/09/2023 Jijini Dar
es Salaam.
Mhe. Balozi
Dkt. Pindi Chana akiongea alipokutana na Balozi wa Urusi nchini Mhe. Andrey
Avetisyan. 27/09/2023 Jijini Dar es Salaam.
XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi
Dkt. Pindi Chana amekutana na Balozi wa Urusi nchini Mhe. Andrey
Avetisyan na kufanya majadiliano ya namna bora ya kuendelea kushirikiana na
Tanzania katika maeneo mbalimbali hasa katika Sekta ya Sheria.
Kikao hicho kimefanyikia tarehe
27/09/2023 katika Ukumbi wa Ofisi za Wakala wa Usajili, Udhamini na Ufilisi
(RITA) Jijini Dar es Salaam ambapo moja ya eneo lililogusiwa katika mazungumzo
hayo ni kuimarisha mifumo ya Haki ambapo Balozi Avetisyan ameahidi kuendelea
kutoa ushirikiano katika maeneo ya kisheria nchini na kusaidia katika
uboreshaji wa sheria.
Katika majadiliano hayo Kwa
upande wa Tanzania, Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana amesema Tanzania
inaendelea kutekeleza Mipango mbalimbali chini ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu
Hassan ikiwemo Kampeni maarufu ya Mama Samia Legal Aid inayolenga kuwasaidia
Watanzania kufikiwa na haki, usajili wa matukio muhimu ya binadamu ikiwemo
vizazi, ndoa na vifo lengo likiwa ni kuhakikisha huduma inafika kwa Wananchi
huku Wizara yake ikisimamia Utawala wa Kisheria na
masuala ya usuluhishi.
Comments
Post a Comment