DKT. CHANA AFANYA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA SINGAPORE NCHINI
Waziri wa Katiba na Sheria
Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akifanya mazungumzo na Balozi wa Singapore nchini
Mhe. Douglas Foo, tarehe 20 Novemba,
2023 mtumba, Jijini Dodoma.
Waziri wa Katiba na Sheria
Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akikabidhi Balozi wa Singapore nchini Mhe. Douglas
Foo mfuko maalum ambao ni rafiki wa mazingira unaotumika kwenye “Mama Samia
Legal Aid Campaign” tarehe 20 Novemba, 2023 Dodoma.
Waziri wa Katiba na Sheria
Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana na Balozi wa Singapore nchini Mhe. Douglas Foo
kwenye picha ya pamoja na washiriki kwenye kikao kilichowakutanisha viongozi
hao wawili, tarehe 20 Novemba, 2023 Dodoma.
XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX
Na William Mabusi – WKS Dodoma
Waziri wa Katiba na Sheria
Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana amekutana na Balozi wa nchi ya Singapore nchini
Mhe. Balozi Douglas Foo na kufanya mazungumzo kuhusu kuimarisha ushirikiano
kwenye sekta mbalimbali na namna ya kubadilishana uzoefu kwenye masuala ya teknolojia.
Kikao hicho kimefanyika tarehe
20 Novemba, 2023 ofisi za Wizara Mtumba kwa lengo la kuendeleza ushirikiano
baina ya nchi mbili hizo.
“Kama Wizara maeneo ya
kubadilishana uzoefu ni kwenye sekta ya sheria, kuendeleza watumishi kwenye
mafunzo mbalimbali. Aidha, tunaangalia namna ya kuimarisha ushirikiano wa kibiashara.”
Alisema Dkt. Chana.
Katika kusimamia utawala wa
sheria, Dkt. Chana amesema Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt.
Samia Suluhu Hassan imeendelea na jitihada za kuongeza uelewa wa sheria kwa
wanachi na hasa wa hali ya chini kwa kuwapa elimu na huduma za kisheria kwa
wasioweza kumudu gharama za Mawakili kupitia kampeni ya kitaifa ya mama Samia.
Katika hatua nyingine Dkt.
Chana amesema Serikali imekuwa ikisisitiza wananchi kutatua migogoro kwa njia
mbadala ya maridhiano ambako huokoa muda kwani mashauri humalizika kwa haraka
bila wahusika kufikishana mahakamani.
Kwa upande wake Balozi wa
Singapore amesema nchi yake itaendelea kuenzi uhusiano mzuri uliopo kati ya
nchi yake na Tanzania na kusema kuwa Singapore iko tayari kuingia makubaliano
ya kibiashara na Tanzania, miongoni mwa mengine.
Comments
Post a Comment