KASI YA UJENZI IENDANE NA UBORA: DKT. CHANA
Mhandisi Nassiri Nassoro akitoa maelezo ya maendeleo ya
ujenzi wa jengo la Wizara kwa Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Pindi
Chana, tarehe 17 Novemba, 2023
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana
akikagua maendeleo ya ujenzi wa jengo la ofisi za Wizara, tarehe 17 Novemba,
2023
XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX
Na William Mabusi –
WKS Dodoma
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana
amekagua maendeleo ya ujenzi wa jengo la ofisi za Wizara ambao umefikia
asilimia 79 linaojengwa Mji wa Serikali Mtumba Dodoma, na kumtaka Mkandarasi
kuongeza kasi huku akizingatia ubora.
Ukaguzi huo ameufanya tarehe 17 Novemba, 2023. “Kwenye
ujenzi wa majengo haya tunashindana hivyo ukiona mwenzio ameweka vioo nawe
unajiuliza la kwangu linawekwa vioo lini,” alisema Dkt. Chana huku
akitahadharisha pamoja na mambo mengine upatikanaji wa maji kwenye jengo
akitaka kuwepo na uwiano wa idadi ya watumishi na uwezo wa pampu ya kusukumuia
maji ili yafike kwenye sakafu zote za jingo
Comments
Post a Comment