MAHAKAMA YA MWANZO YA TARAFA YA BWAKILA CHINI KUJENGWA – MHE GEKUL
Na, George Mwakyembe- WKS – Dodoma.
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Pauline Gekul amefafanua kuwa Serikali katika mwaka fedha 2023/ 2034 imejipanga kujenga Mahakama zaidi ya 60 nchini na katika idadi hiyo pia ipo mahakama ya mwanzo ya tarafa ya Bwakila chini.
Mhe
Gekul ameyasema hayo leo tarehe 07/11/2023 bungeni jijini Dodoma alipokuwa
akijibu swali la mbunge wa Morogoro Kusini Mhe Innocent Edward Kalongoles
alitetaka kujua ujenzi wa mahakama katika eneo hilo utafanyika lini. Mhe Gekul
amefafanua kuwa tayari zabuni imetangazwa kwa ajili ya kumpata mkandarasi wa
ujenzi wa mahakama hiyo na wakati wowote atatangazwa na kuanza kazi.
Aidha,
Mhe Gekul ameleza kuwa Mahakama ya mwanzo ya Matombo na Namvua zina majengo ya
ambayo ni chakavu na tayari Serikali imeyaweka katika mpango wa ukarabati
katika mwaka wa fedha 2024/2025 mpango ambao utajumisha na ukarabati wa Mahakama
zingine nchini.
Pia
Mhe. Gekul ameongeza kuwa Serikali ya awamu ya Sita chini ya Rais Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan imetoa ziadi ya
billion 88 kwa ajili ya ukarabati na ujenzi wa Mahakama ili haki ipatikane kwa
wakati. Hivyo amemtoa wasiwasi mbunge huyo wa Mororgoro kusini na kuhaidi kuwa
Mahakama itajengwa kwa wakati.
Comments
Post a Comment