MHE CHANA ASHIRIKI MKUTANO WA TANZANIA - RUSSIA ALUMNI
Baadhi wa watanzania waliosoma nchini Urusi wakiwa kwenye kikao cha Tanzania -Russia Alumni kilichofanyika Dar es salaam leo tarehe 08 Novemba 2023.
XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe, Balozi Dkt. Pindi Chana ameshiriki Mkutano wa Wanafunzi
waliohitimu Vyuo vikuu vya Nchini Urusi uliofanyika Leo November 08, 2023
jijini Dar es salaam.
Akizungumza katika mkutano huo, Mhe. Chana ameipongeza Urusi
kwa kuendeleza ushirikiano mzuri na Vyuo vya Tanzania katika Kuboresha Elimu na
kuwakaribisha zaidi kuwekeza Tanzania kwani ni sehemu salama.
Aidha,kwa upande wake
Balozi wa Urusi Nchini Andrey Avetsyan amewataka watanzania kujitokeza
kwa wingi kwenda kusoma Nchini Urusi ili kudumisha ushirikiano kati Tanzania na
Urusi kwa kubadilishana ujuzi katika tasnia mbalimbali.
Comments
Post a Comment