MHE. CHANA ATEMBELEA KITUO JUMUISHI CHA MASUALA YA FAMILIA.
Waziri wa
Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana kwenye picha ya pamoja na badhi
ya watumishi wa Kituo Jumuishi cha Masuala ya Familia Temeke, tarehe 15 Novemba
2023.
Naibu
Msajili Mfawidhi Kituo Jumuishi Masuala ya Familia Temeke, Mhe. Frank Moshi
akimpa maelezo Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Pindi Chana alipotembelea Kituo
Jumuishi cha Masuala ya Familia Temeke, 15 Novemba, 2023 Jijini Dar es Salaam.
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana, tarehe 15 November 2023 ametembelea Kituo Jumuishi cha Masuala ya Familia Temeke kukagua shughuli mbalimbali za kiutendaji.
Akiwa Kituoni hapo Waziri Chana amepata fursa ya kutembelea maeneo mbalimbali ikiwemo Chumba maalumu ambacho kimetengwa kwa ajili ya akina mama kunyonyesha watoto wachanga wanapofika katika Kituo hicho kupata huduma.
Comments
Post a Comment